Like Us On Facebook

MWANAUME MMOJA MBARONI KWA KUMBAKA MBUZI.

              Mtu mmoja anaye sadikiwa kuwa na umri wa miaka 23  amefikishwa katika kituo cha polisi cha Nyeri baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka mbuzi katika kijiji cha Ngagirithi huko nchini kenya.

mtuhumiwa huyo wakati akihojiwa na polisi alikiri kutenda tukio hilo na kusema kwamba alimfunga mnyama huyo kwenye mti usiku na kumfanyia kitendo hicho. 

Mbuzi huyo ni mali ya bibi yake.Akielezea mkasa huo bibi huyo alisema "Wakati  nimelala nilisikia vurugu kama vile kuna mtu anijitahidi kumtoa mbuzi kutoka ndani,".

Nilipo amka, nikamkuta mjukuu wangu amevaa shati peke yake.Nikamuuliza kuna tatizo gani, akasema nilikuwa nimekuja kumwangalia mbuzi baada kusikia vurugu.

Wangui(bibi) alisema hakujua mjukuu wake kama alikuwa na mipango ya kufanya kitendo hicho cha kuhuzunisha.

Pia ilibainika kuwa mjukuu huyo amekuwa na tabia mbaya tangu alipokimbia kutoka Kitale miaka miwili iliyopita.

Bibi huyo alisema mjukuu wake alikimbia kitale baada ya "kujaribu kukunyonga baba yake kabla ya kuja kuishi nae. Naamini amekuwa uvutaji bangi,'' alisema.

mtuhumiwa huyo alikutwa akifanya kitendo hicho na jirani yake, ambaye baada ya kusikia kilio cha mbuzi huyo alikuja kuangalia ni kitu gani kilicho msibu ndipo alipo mkuta mjukuu huyo akifanya yake.

mtuhumiwa baada ya kukutwa akifanya hiyo aliamua kukimbia lakini alikamatwa umbali mfupi na umati wa watu baada ya jirani huyo kupiga kengele.
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari