Like Us On Facebook
Showing posts with label KITAIFA. Show all posts
Showing posts with label KITAIFA. Show all posts

MABASI YA MAJINI KUMALIZA MSONGAMANO WA MAGARI JIJINI DAR!!

  
Serikali, mashirika binafsi na wadau wa usafiri ndani na nje ya nchi wamekuwa wakifanya jitihada mbalimbali kukabiliana na msongamano wa magari katika Jiji la Dar es Salaam.
Msongamano huo ambao unachangiwa kwa kiasi kikubwa na uduni wa miundombinu ikiwemo barabara, umekuwa ni kero kwa wananchi na Serikali kwa jumla.
Serikali imewekeza katika Mradi wa Mabasi Yaendayo Kasi (BRT) na usafiri wa treni ndani ya Jiji la Dar es Salaam kama njia mojawapo ya kumaliza tatizo la msongamano wa magari na foleni.
Msingi wa tatizo
Chanzo kikubwa cha foleni jijini Dar es Salaam si wingi wa abiria bali ni wingi wa magari binafsi na njia finyu zisizokidhi mahitaji ya watu walioko katika jiji hilo.
Njia muhimu ya kupunguza foleni na msongamano wa magari ni kupunguza wingi wa magari barabarani na kuweza kuzipanua barabara ili kuwe na uwezekano wa kupita kwa urahisi.
Kutokana na foleni na uduni wa huduma za usafiri wa umma watu wa kundi la kati, wamekuwa wakikimbilia kununua magari binafsi kwa ajili ya kwenda nayo kwenye shughuli zao kwa urahisi.
Aidha, katika kuendeleza harakati za kupambana na tatizo la usafiri, Kampuni ya Transevents Marketing ya Tanzania kwa kushirikana na Kampuni ya Dutch Amphibious Transport Vehicles (DATV) ya Uholanzi inaendelea na mchakato wa kuleta usafiri wa mabasi ya abiria yenye uwezo wa kusafiri nchi kavu na majini.
Mkurugenzi Mtendaji wa Transevents, Peter Nzunda anasema teknolojia hiyo ya mabasi ya nchi kavu na majini (amphibious) ina lengo la kupunguza tatizo la foleni kwenye barabara za Dar es Salaam hususan katikati ya jiji kwa kuwa mabasi hayo huweza kupita nchi kavu na majini.
Hii ina maana kuwa hata katika maeneo yenye barabara zisizo nzuri au zenye tope, magari hayo huweza kupita hivyo kutosababisha foleni kama ambavyo hutokea sasa katika baadhi ya maeneo hasa mvua zinaponyesha na kuharibu barabara.
Anasema mbali na lengo hilo, mabasi hayo yatatumika kama vivutio vya utalii kwa kufanya utalii wa baharini ambao kwa Tanzania haujashika kasi, licha ya sehemu kubwa ya nchi kuzungukwa na maji.
“Mpango huo wa mabasi ya nchi kavu na majini unalenga kutoa ushawishi kwa watu wa kundi la kati ambao wanatumia magari binafsi waegeshe magari yao na kutumia usafiri huu ambao utakuwa wa hadhi yao na unaokidhi haja kwa ubora wake,” anasema Nzunda na kuongeza:
“Lengo ni kujenga maegesho ya magari maeneo mbalimbali kandokando ya bahari, watu wataegesha magari yao na kupanda mabasi yatakayopita majini kwenda Posta na baadaye kurejea kwa utaratibu huohuo na kuyachukua magari yao tena kwenye maegesho walipoacha magari yao”.
Shughuli za utalii
Nzunda anasema mbali na teknolojia hiyo kutumika kama usafiri wa umma Jiji la Dar es Salaam, mabasi hayo yatatumika kupeleka watalii kwenye hifadhi za taifa zinazozungukwa na maji kama vile Bagamoyo, Mbudia, Mafia na visiwa vingine ili kujionea mambo mengi zaidi ya kiutalii.
“Tunataka pia watu wanaokwenda kwenye fukwe wasiishie kulala na kucheza mchangani, bali wawe wanapanda mabasi haya na kutembelea sehemu  mbalimbali zenye vivutio baharini; hiyo itakuwa ni fursa ya watu kuzunguka baharini wakiwa ndani ya mabasi hayo yatakayokuwa katika miundo tofauti,” alisema Nzunda.
Mahitaji ya mradi
Nje ya Kampuni ya Dutch Amphibious Transport Vehicles (DATV) kutaka kuingiza teknolojia hiyo nchini, Serikali ya Uholanzi pia ipo tayari kuchangia  kwa asilimia 50 ya gharama za mradi wote ambao gharama zake zitajulikana mara baada ya kufanyika tathmini wa mradi.
Aidha, Serikali ya Tanzania, wawekezaji katika sekta ya usafirishaji wa abiria nchi kavu na majini na wadau wengine watatakiwa kuchangia asilimia 50 zilizobaki katika kufanikisha kuanza kwa mradi huo ambao mchakato wa kupata kibali umeshaanza.
Meneja Mwendeshaji wa Transevents Marketing, Mahamud Omari anaiomba Serikali kusaidia uharakishaji wa utoaji wa leseni ya uingizwaji wa teknolojia hiyo mpya ya mabasi.
“Mchakato wa kupata kibali umeshaanza na matarajio yetu ni kufanikisha hatua hiyo baada ya miezi sita kuanzia sasa,” anasema Omari.
Ofisa Uhusiano wa kampuni hiyo, Edna Rebecca anasema mradi huo wa ‘Mabasi ya Majini na Nchi Kavu’ utatengeneza ajira nyingi kwa vijana wengi na kuongeza fursa za kibiashara kwenye hoteli.
Pia mabasi hayo yataongeza pato la taifa kupitia utalii na maendeleo ya teknolojia hiyo kwa jumla, kwa ajili ya kizazi hiki na kijacho, ukizingatia takwimu za Shirika la Makazi Duniani, zinaonyesha miaka 50 ijayo, Jiji la Dar es Salaam litakuwa na wakazi wapatao milioni 18.
Mabasi hayo yatatumika kwa shughuli za harusi hasa kwa wanandoa ambao watapenda kufunga ndoa ndani ya maji.Pia yatatumika kwa safari za kitalii za wafanyakazi wa kampuni mbalimbali, wanafunzi, wanakwaya, wanavikundi na klabu za mipira.
“Usafiri huu utakuwa ni wa bei ya kati ambayo itaendana na huduma bora na utalenga kuziba changamoto zote ambazo zinapatikana sasa kwenye usafiri mwingine wa umma,” anasema Rebecca na kuongeza:
“Kuna watu wanapanda magari kwa kulipia Sh1,000 badala ya Sh400 kutoka Posta kwenda Mwenge ili kukwepa adha ya kubanana kwenye daladala zinazokaa muda mrefu kwenye foleni, kwahiyo unaweza kuona ni kwa namna gani watu wanahitaji huduma bora za usafiri wa umma.”
Katika mazingira ya kawaida familia nyingi jijini Dar es Salaam zinatumia magari matatu kwa wakati mmoja yaani baba, mama na mtoto, jambo linaloongeza masongamano barabarani.
Rebecca anasema usafiri huo utawafanya watu hao kuyaacha magari yao nyumbani au kwenye maegesho ya magari yatakayojengwa na hivyo kupunguza kabisa idadi ya magari barabarani.
Mabasi hayo pia yatapunguza gharama za maisha zinazotokana na matumizi ya mafuta kwani kama mtu anaweza kutumia lita 20- 50 kwa siku.
Serikali inasemaje
Meneja Mawasiliano wa Mamlaka ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), David Mziray anasema teknolojia hiyo ya usafiri wa mabasi ya nchi kavu na majini imekuwa na msaada mkubwa kwa nchi nyingi Ulaya, kuja kwake Tanzania itakuwa ni habari njema hususan wakati huu ambapo jiji linakua kwa kasi.
 “Kazi yetu ni kupokea maombi na kuangalia kama yanakwenda sambamba na sheria na kanuni zetu na kama unavyojua hii ni aina mpya ya usafiri kwa hiyo lazima kutakuwa na mambo ya msingi ya kuyajadili na kuyapatia ufumbuzi kabla ya kuanza,” Anasema Mziray
Baadhi ya wananchi wanasema mradi huo unaweza kusaidia sana kuondoa kero ya usafiri Dar es Salaam.
-Mwananchi

UNYAMA: KIJANA AUA MAMA YAKE KWA JEMBE HUKO KAHAMA,TUNAOMBA RADHI KWA PICHA

Katika hali ya kusikitisha ,kuhuzunisha na isiyokuwa ya kawaida kijana mmoja mkazi wa kijiji cha Mwakuhenga wilayani Kahama mkoani Shinyanga amemuua mama yake kwa kumkata na jembe kichwani na kusababisha kifo chake.
Habari kutoka Kahama zinasema tukio hilo limetokea jana majira ya saa mbili usiku na chanzo halisi cha tukio hilo bado hakijajulikana.

Habari kamili kuhusu tukio hili tutakuletea kupitia kwenye blog hii

CHANZO: MALUNDE BLOG

JE UMETAFUTA KAZI KWA MUDA MREFU BILA MAFANIKIO?KAZI HIZI HAPA SASA CHAGUA INAYOKUFAA!



  GRAPHIC DESIGNER, TANZANIA     
Qualifications: National Diploma or degree in Design
 Details:Daily News 10 Feb 2014
Deadline: 21  February , 2014

SCIENCE EDITOR, TANZANIA     
Qualifications: Bachelor’s degree in Science with Education (majors Chemistry and Biology)
Apply: oxfordtz@oup.com
Details:Daily News 10 Feb 2014
Deadline: 21  February , 2014

SALES  EXECUTIVE, TANZANIA     
Qualifications: A relevant degree or Diploma in Sales & Marketing
Apply: oxfordtz@oup.com
Details:Daily News 10 Feb 2014
Deadline: 21  February , 2014

CLIENT OPERATIONS MANAGER     
Qualifications: Degree in Business  Administration or equivalent, at least 5 years experience in clearing and forwarding
Apply: carees.tanzania@bollore.com
Details:The Guardian 14 Feb 2014
Deadline: 21  February , 2014

CUSTOMS RISK MANAGER     
Qualifications: Degree in Business Administration or equivalent ITA Certificate or similar certificates
Apply: carees.tanzania@bollore.com
Details:The Guardian 14 Feb 2014
Deadline: 21  February , 2014

SALES REPRESENTATIVE - 4 POSTS     
Qualifications: University degree or Diploma from a reputable higher learning institution
Apply:Head of Human Resources Total Tanzania Limited
Box 1503, Dar es Salaam
Details:Mwananchi 14 Febr 2014
Deadline: 28  February , 2014

DRIVERS     
Qualifications: Education level shall be minimum Form IV level (Ordinary Certificate of Seconadary Education
Apply: Human Resources Department Box 95068, Dar es Salaam
Details:Mwananchi 14
February 2014
Deadline: 24  February , 2014

SENIOR  LECTURER     
Qualifications: Holder of a PhD in a specialised functional area with at least nine years of work experience related to teaching and/or research
Apply: The Deputy Vice Chancellor (Administration and Finace)Box 1, Mzumbe
Details:Mwananchi 14 Febr 2014
Deadline: 06  March, 2014

SENIOR  RECORDS MANAGEMENT  ASSISTANT  II   
Qualifications: Holder of a Diploma in Records management from a recognised institution with working experience of at least six years
Apply: The Deputy Vice Chancellor (Administration and Finace)Box 1, Mzumbe
Details:Mwananchi 14 Febr 2014
Deadline: 06  March, 2014

SENIOR  LIBRARY  ASSISTANT     
Qualifications: Holder of a Diploma in Library and Information studies from any recognised institution with working experience of at least six years
Apply: The Deputy Vice Chancellor (Administration and Finace)Box 1, Mzumbe
Details:Mwananchi 14 Febr 2014
Deadline: 06  March, 2014

SENIOR  WEB OFFICER    
Qualifications: Bachelor’s degree in Science,Communication,Public Relations,Technical writing or related field
Apply: Director of Human
Resources CRDB Bank
Box 268, Dar es Salaam
Details:The Guardian 10
Febuary 2014
Deadline: 01  March, 2014

SALES MANAGER     
Qualifications: Bachelor’s degree or its equivalent in Business Administration with biases in Marketing and sales,Possesion of postgraduate or  Master’s degree will be an added advantage
Apply: Director of Human
Resources CRDB Bank
Box 268, Dar es Salaam
Details:The Guardian  10
February 2014
Deadline: 01  March, 2014

HEALTH ADVOCACY AND ENGAGEMENT DIRECTOR   
Qualifications: Master’s degree
 in Public Health,Health Economics,Health Policy or a related field PhD,MD or Dr Ph preferred  
Apply:Country Human Resources Manager Plan International Tanzania
Box 3517, Dar es Salaam
Details:The Guardian 13Feb 2014
Deadline: 28 February, 2014

MANAGER CALL  CENTRE    
Qualifications: Degree/Advanced Diploma or its equivalent in Business Administration from
 a recognised training institution,
Possesion of a Master’s degree
 will be an added advantage
Apply: Director of Human
Resources CRDB Bank
Box 268, Dar es Salaam
Details:The Guardian 10 Feb 2014
Deadline: 01  March, 2014

GEOGRAPHICAL  INFORMATION SYSTEM (GIS) EXPERT
Qualifications: A Holder of degree or Advanced Diploma in Land surveying/Planning/Information Technology/Geography with emphasis in GIS or should have pursued a Certificate or Diploma program in GIS
Apply: The Managing Director Arusha Urban Water Supply and Sewerage Authority
Box 13600, Arusha
Details:The Guardian 11 Febr2014
Deadline: 28  February, 2014

PROJECT  ENGINEER    
Qualifications: A Holder of Bachelor Science degree/Advanced Diploma in Civil/Sanitary/Environmental Engineering from a recognised higher learning Institution
Apply: The Managing Director Arusha Urban Water Supply and Sewerage Authority
Box 13600, Arusha
Details:The Guardian 11 Febr2014
Deadline: 28  February, 2014

CHIEF  MANAGER - HUMAN
RESOURCES  &  ADMINISTRATION    
Qualifications: Holder of Master’s degree in Public Administration, Human Resource Management or Business Administration
Apply: The Managing Director DCB Commercial Bank Ltd
Box 19798, Dar es Salaam
Details:The Guardian 13Febr2014
Deadline: 25  February, 2014

ACCOUNTANT GRADE II    
Qualifications: Holder of a Full professional qualification i.e. CPA,(T),ACCA,ACA,ICMA and has been registered with NBAA
Apply: The Deputy Vice Chancellor (Administration and Finace)Box 1, Mzumbe
Details:Mwananchi 14 Febr 2014
Deadline: 06  March, 2014

FINANCE AND ADMINISTRATION DIRECTOR  
Qualifications: Master’s degree
 in finance or financial Management and/or a professional qualification in Accountancy
Apply:Country Human Resources Manager Plan International Tanzania
Box 3517, Dar es Salaam
Details:The Guardian 13Febr2014
Deadline: 28 February, 2014

CHIEF OF PARTY
Qualifications: Master’s degree
 in Public Health,Health Economics,Health Policy or a related field PhD,MD or Dr Ph preferred
Apply:Country Human Resources Manager Plan International Tanzania
Box 3517, Dar es Salaam
Details:The Guardian 13
Febr2014
Deadline: 28 February, 2014

FUNDRAISING OFFICER
Qualifications: Degree in Business Management,Project Management,Public relations Mass Communication,Business Law,or a related field preferred
Apply: The Executive Director PASADA
Box 70225, Dar es Salaam
Details:Daily News 13
Febr, 2014
Deadline: 15 March, 2014

DIVERS - 2 POSITIONS
Qualifications: Secondary School and know how to read,write and count; must posses a valid Tanzania driver’s licence class ‘C’
Apply: The Executive Director PASADA
Box 70225, Dar es Salaam
Details:Daily News 13
Febr, 2014
Deadline: 15 March, 2014

ASSISTANT  MEDICAL  OFFICER - 2 POSITIONS
Qualifications: Advanced Diploma in clinical Medicine and registered as a qualified medical practitioner
Apply: The Executive Director PASADA
Box 70225, Dar es Salaam
Details:Daily News 13
Febr, 2014
Deadline: 15 March, 2014

MEDICAL DOCTORS - 2 POSITIONS
Qualifications: A Medical degree (MBBS),MB,or MD) and registered as a qualified medical practitioner  in Tanzania
Apply: The Executive Director PASADA
Box 70225, Dar es Salaam
Details:Daily News 13
Febr, 2014
Deadline: 15 March, 2014

SENIOR WATER ENGINEER    
Qualifications: A Holder of Bachelor Science degree/Advanced Diploma in Civil/Sanitary/Environmental Engineering from a recognised higher Learning Institution
Apply: The Managing Director Arusha Urban Water Supply and Sewerage Authority
Box 13600, Arusha
Details:The Guardian 11 Feb 2014
Deadline: 28  February, 2014

HUMAN RESOURCES AND ADMINISTRATIVE OFFICER
Qualifications: Bachelor’s degree in Human Resource Management or equivalent
Apply: Human Resources and Administrative Manager
Box 10160, Dar es Salaam
Details:The Guardian 13Febr2014
Deadline: 28 February, 2014

COMMUNITY DEVELOPMENT OFFICER II - 4  POSITIONS
Qualifications: Holder of a degree in Sociology,Social work and Community Development from a recognised institution with 1st class or upper 2nd class or Master’s degree in a relevant field
Apply: Tanzania Petroleum
Development  Corporation
Benjamin W. Mkapa Tower
Box 2774, Dar es Salaam
Details:Daily News 3 Febr, 2014
Deadline:  February, 2014

ADMINISTRATIVE OFFICER II - 2  POSITIONS
Qualifications: Holder of a degree in Public Administration from a recognised institution with 1st or upper 2nd class Master’s degree in a relevant field
Apply: Tanzania Petroleum
Development  Corporation
Benjamin W. Mkapa Tower
Box 2774, Dar es Salaam
Details:Daily News 3 Febr, 2014
Deadline:  February, 2014

LABORATORY TECHNICIAN II - 4  POSITIONS
Qualifications: Holder of a Diploma in Laboratory Technology from a recognised institution followed by at least 2 years post
 -qualification experience
Apply: Tanzania Petroleum     
Development  Corporation
Benjamin W. Mkapa Tower
Box 2774, Dar es Salaam
Details:Daily News 3 Febr, 2014
Deadline:  February, 2014

INSTRUMENTATION ENGINEER II - 8  POSITIONS
Qualifications: BSc. in Instrumentation Engineering or related field with 1st class or upper 2nd class or Master’s degree in Economics
Apply: Tanzania Petroleum
Development  Corporation
Benjamin W. Mkapa Tower
Box 2774, Dar es Salaam
Details:Daily News 3 Febr, 2014
Deadline:  February, 2014

MARKETING OFFICER II -2  POSTS
Qualifications: Holder of a Bachelor’s degree in Marketing with 1st class or upper 2nd class Apply: TPDC
Benjamin W. Mkapa Tower
Box 2774, Dar es Salaam
Details:Daily News 3 Febr, 2014
Deadline:  February, 2014
MONITORING AND EVALUATION OFFICER
Qualifications: Master’s degree in Public Health,Epidemiology,Demograhpics or a related field
Apply: Director of Human Resource and Admistration Pathfinder International
Box 77991, Dar es Salaam
Details:Daily News 14 Febr, 2014
Deadline: 21 February, 2014

COMMUNITY HEALTH PROGRAM OFFICER
Qualifications: Bachelor’s degree /Diploma in Medicine,Public Health,Nursing or equivalent
Apply: Director of Human Resource and Admistration Pathfinder International
Box 77991, Dar es Salaam
Details:Daily News 14 Febr, 2014
Deadline: 21 February, 2014

PROJECT MANAGER
Qualifications: Advanced degree in Public Health,Social Sciences or related field
Apply: Director of Human Resource and Admistration Pathfinder International
Box 77991, Dar es Salaam
Details:Daily News 14 Febr, 2014
Deadline: 21 February, 2014

ASSISTANT INTERNAL AUDITOR
Qualifications: Holder of a degree in Accounting or equivalent qualification from a recognised institution, knowledge in Accounting software will have an advantage
Apply: Director General gaming Board of Tanzania
Box 1717, Dar es Salaam
Details:Daily News 14 Febr, 2014
Deadline: 28 February, 2014

LICENSING OFFICER
Qualifications: Holder of first degree in Law (LLB),Bachelor of Business Administration, B. Com Accounting,B.Com Finance or equivalent qualification from a recognised institution. Holders of LLB degree who are registered as advocates of the High Court will have added advantage
Apply: Director General Gaming Board of Tanzania
Box 1717, Dar es Salaam
Details:Daily News 14 Febr, 2014
Deadline: 28 February, 2014

PRINCIPAL  PROCUREMENT -
OFFICERS - 4 POSITIONS
Qualifications: Bachelor’s degree in Procurement and Materials Management from recognised higher institutions, Master’s degree in a relevant field will be an added advantage
Apply: Senior Manager, Human Resources Tanesco Umeme Park
Box 9024, Dar es Salaam
Details:Daily News 14 Feb, 2014
Deadline: 28 February, 2014
 
MANAGER PROCUREMENT -TENDE-
RING
Qualifications: Bachelor’s degree in Procurement and Materials Management from recognised higher institutions,Master’s degree in a relevant field will be an added advantage
Apply: Senior Manager Human Resources Tanesco Umeme Park
Box 9024, Dar es Salaam
Details:Daily News 14 Febr, 2014
Deadline: 28 February, 2014

MANAGER PROCUREMENT -CONTRACTS AND COMPLIANCE
Qualifications: Bachelor’s degree in Procurement and Materials Management from recognised higher institution, mMaster’s degree in a relevant field will be an added advantage
Apply: Senior Manager Human Resources Tanesco Umeme Park
Box 9024, Dar es Salaam
Details:Daily News 14 Febr, 2014
Deadline: 28 February, 2014

SENIOR MANAGER PROCUREMENT
Qualifications: University
degree in Business Admini
stration,Procurement and
Commerce
Apply: Senior Manager Human Resources Tanesco Umeme Park
Box 9024, Dar es Salaam
Details:Daily News 14 Febr, 2014
Deadline: 28 February, 2014

SECURITY GUARD - 7 POSITIONS Qualifications: Holder of Form IV with National Service training as an added advantage
Apply: Human Resource
Department of the State
University of Zanzibar
Box 146, Zanzibar
Details: Daily News 30
January, 2014
Deadline: 19 February, 2014

OFFICE ATTENDANT III
Qualifications: Holder of Form IV Certificate or equivalent
Apply: Human Resource
Department of the State
University of Zanzibar
Box 146, Zanzibar
Details: Daily News 30
January, 2014
Deadline: 19 February, 2014

TUTORIAL  ASSISTANT - 2 POSTS
Qualifications: Possession of a first degree from a recognised higher learning institution and must have obtained an upper second class having a minimum GPA of 3.8
Apply: The Chairpeson Search Team,C/oMoshi University College of Co-operatives and Business studies
Box 474, Moshi
Details: Daily News 30
January, 2014
Deadline:  February, 2014
 
LOAN DESK OFFICER
Qualifications: Holder of Bachelor’s degree in Accounting/Finance/Economic/Business Administration/Entrepreneurship or equivalent
Apply: Human Resource
Department of the State
University of Zanzibar
Box 146, Zanzibar
Details: Daily News 30
Jan, 2014
Deadline: 19 February, 2014

OFFICE SUPERINTENDENT  
Qualifications: Holders of Diploma of Human Resource Management /Diploma in Public Administration
Apply: Human Resource
Department of the State
University of Zanzibar
Box 146, Zanzibar
Details: Daily News 30
Jan, 2014
Deadline: 19 February, 2014

ASSISTANT LECTUERS FOR SOCIAL WORK/ARCHAEOLOGY AND HERITAGE/TOURISM/PORTUGUESE
Qualifications: Holder of Master’s degree in relevant areas of study with a GPA of not less than 3.5 or equivalent at undergraduate level
Apply: Human Resource
Department of the State
University of Zanzibar
Box 146, Zanzibar
Details: Daily News 30
Jan, 2014
Deadline: 19 February, 2014

COMPUTER  PROGRAMMER
Qualifications: Holder of first degree in Computer Science, Information systems Telecommunication/Electrical Engineering/Information Technology/GIS or any related Computer studies with at least three years relevant working experience in a similar position
Apply: The Deputy Vice - Chancellor(Academics) Open University of Tanzania
Box 23409, Dar es Salaam
Details: Daily News 27
January, 2014
Deadline:  February, 2014

RECORDS  MANAGEMENT  
ASSISTANT III   
Qualifications: Holder of Form IV/VI Certificate with two Principal Passes in Arts subjects and must have a credit pass in English at “O” level plus a Certificate in Records Management from a recognised institution
Apply: The Deputy Vice - Chancellor(Academics) Open University of Tanzania
Box 23409, Dar es Salaam
Details: Daily News 27
January, 2014
Deadline:  February, 2014

PERSONAL SECRETARY II - 2 POSITIONS
Qualifications: Holder of National Form IV/VI Certificate with credit passes in English and Kiswahili or Foundation Course Certificate plus Diploma in Secretarial studies from TPSC or any recognised institution
Apply: The Deputy Vice - Chancellor(Academics) Open University of Tanzania
Box 23409, Dar es Salaam
Details: Daily News 27
January, 2014
Deadline:  February, 2014

ACCOUNTS ASSISTANT  II
Qualifications: Holder of Form VI Certificate with NABE III/ATECII/Diploma in Accountacy /Module A and plus ICT skills
Apply: The Deputy Vice - Chancellor(Academics) Open University of Tanzania
Box 23409, Dar es Salaam
Details: Daily News 27
January, 2014
Deadline:  February, 2014

ASSISTANT DEAN OF STUDENTS  
Qualifications: Holder of Master’s degree in Education majoring in Guidance and Counselling/social work
Apply: Human Resource
Department of the State
University of Zanzibar
Box 146, Zanzibar
Details: Daily News 30
January, 2014
Deadline: 19 February, 2014

BREAKING NEWS: MAPIGANO MAKALI YANAENDELEA KATIKA ENEO LA MBEZI JUU JIJINI DAR ES SALAAM

 Hili ni kundi la vijana waendesha bodaboda wakienda mtoni kumwokoa mwenzao ambaye wanadai ametekwa na wahuni wanaojificha mtoni na kukaba watu, mpaka sasa boda boda aliyetekwa yupo mwananyamala hospital na mmoja wa vijana wanaoaaminika kwamba ni vibakaba ameshauawa
Kuna mapigano makali eneo la kwa mzee Juma Kata ya Mbezi juu.
Habari zaidi zionasema kwamba Waendesha Bodaboda hao wanaendelea kupambana kwa kutumia silaha za jadi dhidi ya vijana wanaosemekana aidha 
ni vibaka au wameiba pikipiki ya mwenzao.
Hali ni mbaya majeruhi ni wengi na inasemekana kuna vifo vimetokea.
SOURCE:kapinga blog
<<USISAHAU KUBOFYA HAPA ILI UPATE UTAMU WA MJINI>>

KESI YA KIFO CHA KANUMBA... LULU AANIKA UKWELI,MAMA KANUMBA AMWAGA MACHOZI!!

MWANGA umeanza kuonekana juu ya kesi inayomkabili staa wa filamu za Bongo, Elizabeth Michael Kimemeta ‘Lulu’ ya kumuua bila kukusudia staa mwenzake wa muvi, Steven Charles Meshack Kusekwa Kanumba ambapo safari hii aliamua kukiri vipengele kibao, Risasi Mchanganyiko lina habari yote.
Elizabeth Michael 'Lulu' aliyeambatana na Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’ wakiwa eneo la mahakama.
Akikiri mbele ya Mahakama Kuu ya Tanzania juzi (Jumatatu) wakati kesi hiyo ilipoanza kusikilizwa, nyota huyo aliweka wazi mambo ambayo hapo awali hakuwahi kuyakubali kortini jambo lililovuta hisia za wasikilizaji waliokuwa wamefurika ndani ya chombo hicho cha kutoa haki kujua kinachoendelea.
Mwendesha mashitaka wa upande wa serikali, Monica Mbogo alivitaja vipengele kadhaa ambavyo Lulu alitakiwa kuvikana au kuvikubali.
Lulu, mama yake mzazi Lucresia Karugila wakiongea na mwanasheria wao, Peter Kibatala mahakamani.
Katika kesi hiyo iliyoendeshwa kwa ustadi mkubwa wa wanasheria kuoneshana ujuzi wa kusoma na ‘kubugia’ vipengele vigumu vya sheria, Lulu alipata wakati mgumu wa mambo kiasi cha kumwita wakili wake, Peter Kibatala mara kwa mara.
MADAI YA KUMUUA KANUMBA BILA KUKUSUDIA
Lulu alikiri kwamba, mashitaka yake mahakamani hapo yalikuwa ya kumuua bila kukusudia, marehemu Steven Kanumba Aprili 7, mwaka 2012.

Lulu akiongea na mama yake kabla kesi yake kuanza kusikilizwa.
KUWEPO ENEO LA TUKIO NA KUTOKEA KWA UGOMVI
Katika maelezo yake, Lulu aliweka bayana kuwa siku ya tukio alifika nyumbani kwa marehemu maeneo ya Sinza ya Vatican jijini Dar saa 6 usiku na kuingia moja kwa moja chumbani.
Alizidi ‘kuchezesha taya’ kuwa, kulitokea ugomvi kati yake na marehemu licha ya kutotaja chanzo cha ugomvi huo.

Aliongeza kwamba, Kanumba alimvuta mkono na kumrudisha ndani wakati alipokuwa akijaribu kukimbia na kuufunga mlango, mwishowe alifanikiwa kutoka na kukimbia kusikojulikana.
KUKAMATWA KWAKE BAMAGA
Lulu aliweka wazi kuwa, siku ya tukio, saa 11alfajiri alikamatwa maeneo ya Bamaga- Mwenge jijini Dar es Salaam alipokuwa akijaribu kutorokea kusikojulikana.

KUHUSU UHUSIANO
Bila kupepesa macho wala kuchezesha kope, Lulu alikubali kuwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na marehemu Kanumba kwa muda ambao hakuutaja hali ambayo baadhi ya watu walionesha kuwa ‘sapraizidi’.

AMWAGA MACHOZI KORTINI
Awali, Lulu alipofika mahakamani hapo akiwa ameongozana na mama yake mzazi, Lucresia Karugila na staa wa muvi za Kibongo, Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’ alionekana kuwa na amani.

Msanii huyo alimudu kusoma Gazeti la Ijumaa Wikienda ambalo liliingia mtaani siku hiyo. Lakini baada ya kuanza kwa kesi, ilifika mahali alidondosha machozi hali iliyomlazimu kujifuta uso kwa kitambaa.
Baadhi ya watu walinong’ona kuwa, mrembo huyo alikuwa analizwa na kumbukumbu za tukio la kifo cha Kanumba na kwa sababu ya kuogopa kesi.

MAMA KANUMBA ASUSA
Habari nyingine zilidai kuwa, mama wa marehemu Kanumba, Flora Mtegoa hakutokea mahakamani hapo licha ya umoja na udugu alionao kwa sasa na familia ya  Lulu.

Ilidaiwa kuwa sababu kubwa ya kushindwa kufika kortini ni kukosa uamuzi wa upande gani angekaa kati ya mshtakiwa (Lulu) na mshitaki (Jamhuri) kwa vile kote kuna muhusu kwa sasa.
“Unajua mama Kanumba alipogundua kwamba anayetakiwa kujibu madai ni Lulu ambaye baada ya kutoka mahabusu alimtangaza ni mwanaye na anayelalamika ni serikali, alishindwa kujua akija leo (juzi) angekaa upande gani? Akaamua kutokufika kabisa,” kilisema chanzo chetu.
Risasi Mchanganyiko lilimsaka kwa simu mama huyo lakini bila mafanikio kufuatia simu yake ya mkononi kuita muda mrefu bila kupokelewa.
TUJIKUMBUSHE KIDOGO
Lulu alikamatwa kwa kosa la kumuua bila kukusudia aliyekuwa galacha wa filamu za Kibongo, marehemu Steven Kanumba mnamo Aprili 7, 2012 nyumbani kwake, Sinza Vatican jijini Dar.

Baada ya kukamatwa na kuswekwa mahabusu ya Kituo cha Polisi Oysterbay jijini Dar, Lulu alipandishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambapo hakutakiwa kujibu ndiyo au hapana.
Hata hivyo, ilielezwa kuwa mahakama hiyo haikuwa na uwezo wa kusikiliza kesi ya madai hayo.
Aliachiwa kwa dhamana Januari 29, 2013 na kuambiwa kwamba kesi yake itakaporudi, itakuwa chini ya mahakama kuu. Juzi ilianza kusikilizwa kwa mara ya kwanza.

-GPL

BAADA YA KUTANGAZA KURUDI SHULE,CHEKA AANZA UTORO SHULENI!

Bondia Francis ‘SMG’ Cheka, amedaiwa kuingia darasani siku moja tu tangu aliposajiliwa kama mwanafunzi mpya wa Chuo cha St Joseph cha mjini Morogoro Septemba mwaka jana.
Akizungumza na MWANANCHI, mwalimu wa Cheka aitwaye Mkisi amesema Cheka ameomba kuendelea na masomo baada ya kutoonekana darasani kwa miezi kadhaa bila taarifa yoyote, na kubainisha kuwa hawawezi kumruhusu kuingia muhula wa pili.
Cheka alipewa ufadhili wa masomo chuoni hapo mwaka jana mara baada ya kutwaa ubingwa wa dunia wa WBF Agosti 30, baada ya kumpiga Phil Williams wa Marekani katika pambano lililofanyika jijini Dar es Salaam.
Mkisi amesema kuwa bondia huyo amekosa vipindi kwa muda mrefu hivyo hawezi kuingia muhula mwingine, kwakuwa atakosa vitu vingi hivyo anapaswa kujisajili kama mwanafunzi wa muhula mpya utakaoanza Machi 24.
“Cheka aliingia darasani siku moja na ‘kupotea’ hata hivyo hivi karibuni alikuja na kutuambia anataka kuendelea na shule ingawa hatuwezi kumuendelezea programu yake ya awali,” alisema Mkisi.
-Mwananchi

LOWASSA NA WENZAKE SITA WAPEWA ONYO KALI NA CCM

Press Conference ya CCM imefanywa na Nape saa 8.... Issue ni kwamba wale vigogo 6 wa CCM wamepewa onyo kali, karipio na kwa maana hiyo watakuwa chini ya uangalizi maalumu kwa miezi 12 kuanzia jana kutogombea nafasi yoyote ya uongozi ndani ya CCM... Lowassa, Ngeleja, Membe, Wasira, Januari, Sumaye... Uwezekano wa kugombea nafasi ya urais yaota mbawa?
-udaku special

MHHH HATARI: UTAJIRI WA MBUNGE WA CCM "VICKY KAMATA" NI BALAA..KANUNUA HADI MGODI,CHEKI MWENYEWE HAPA


WANAWAKE na maendeleo, tufanye kazi, tusonge mbele, yelele…yelele… Hii sehemu ya mashairi ya wimbo wa staa wa muziki wa kizazi kipya na Mbunge wa Viti Maalum (UVCCM), Geita, Vicky Kamata anayetajwa kuwa na utajiri balaa.


Mbunge wa Viti Maalum (UVCCM), Geita, Vicky Kamata.
UWAZI LINA KILA KITU
Vicky amepata mafanikio makubwa ambayo kila mwanamke Tanzania angependa kuyapata. Gazeti hili lilimchimba kwa kina na kupata utajiri wote alionao kwa sasa.

KABLA YA SIASA, KABLA YA BONGO FLEVA
Kabla ya siasa aliishi maisha ya dhiki ambayo hakutegemea kama angekuja kupata mafanikio makubwa. Ni miongoni mwa Watanzania waliozaliwa katika familia duni.
Katika kutafuta ‘kutoka’ kimaisha, Vicky amewahi kuwa mwanamuziki wa Bongo Fleva na kutunga nyimbo mbalimbali, wimbo wa Wanawake na Maendeleo ndiyo uliomtambulisha zaidi katika jamii.

“Nimezaliwa kwenye familia duni, nimeishi maisha ya dhiki sana, mbali na muziki, nimewahi kuwa mwalimu wa shule ya msingi kule Moshi (Kilimanjaro) katika harakati za kusaka maisha, baadaye nilikwenda Morogoro.
“Kila kitu kinabadilika kama ukimwamini Mungu,” alisema Vicky mwenye watoto wawili, Revocatus na Glory (jina la baba halikutajwa).
MAFANIKIO YAANZA
Mwaka 2006, Vicky alifanikiwa kuajiriwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) akiwa ni afisa uhusiano.
Mwaka 2010, Vicky alifanikiwa kuwa mbunge wa viti maalum akiuwakilisha Mkoa wa Geita.

MJENGO WA GHOROFA MBILI
Akiwa mbunge, Mheshimiwa Vicky ameingia kwenye orodha ya wanawake mabilionea nchini kwa kuangusha mjengo wa kifahari wa ghorofa mbili Sinza jijini Dar es Salaam wenye thamani ya shilingi bilioni moja na milioni mia nne.

Ndani ya ghorofa hilo kuna bwawa la kisasa la kuogelea ‘swimming pool’ ambalo linatumiwa na familia yake.
MAGARI YAKE SASA
Kama walivyo matajiri wengine, mheshimiwa huyo anamiliki magari manne ya kifahari, yote yakiwa na thamani ya shilingi milioni 261.
Ana Toyota Voxy- Noah ambalo alilitoa sokoni kwa shilingi milioni 16.
Kamata pia anamiliki BMW X5 likiwa na thamani ya shilingi milioni 130.

Mara nyingi anapokwenda bungeni, Vicky hutembelea gari linalomudu mikiki ya barabarani, Toyota Land Cruiser ‘VX’ ambalo lina thamani ya shilingi milioni 90.
Pia mwanamama huyo ana gari aina ya Toyota Altezza alilolinunua kwa shilingi milioni 25.

ANAMILIKI MGODI WA DHAHABU
Wakati hayo yakiwa wazi, chanzo makini kilidai kuwa, mheshimiwa huyo amenunua mgodi wa dhahabu Geita, jambo ambalo ni sehemu kubwa ya mafanikio yake.

“Vicky amenunua mgodi wa dhahabu Geita, mimi ni mtu wangu  wa karibu, hapendi kusema mafanikio yake wala watu wajue lakini ukweli ndiyo huo. Eneo ni kubwa, muda si mrefu uchimbaji utaanza,” kilisema chanzo cha habari kwa sharti la kutoandikwa jina gazetini.
ANA SHAMBA LA EKARI 157
Utajiri wa mheshimiwa huyo unaendelea kuanikwa kuwa, ni pamoja na shamba  lenye ekari 150, Kisarawe, Mkoa wa Pwani. Pia ana shamba la miti Kibamba, Dar lenye ekari 7.

NI MFUGAJI
Mbali na mambo mengine, Vicky ni mfugaji kama ilivyo asili ya Wasukuma. Anafuga ndege aina ya kanga, kuku wa kisasa na mbuzi.

ANASOMESHA WATOTO WASIOJIWEZA
Katika mambo ambayo huenda yanachangia kuchota baraka, mheshimiwa Vicky anawalipia ada ya sekondari watoto yatima, walemavu na wasiojiweza kimaisha, idadi yao ikifikia 75.

KIPATO CHAKE KIKOJE?
Dodoso zinaonesha kwamba, kwa kazi ya uheshimiwa, kwa mwezi anaingiza shilingi milioni 15 ukijumlisha posho zote za ubunge, ujumbe wa kamati ya bunge na mshahara.

AMFUNIKA ANNE MAKINDA
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa, jumba la kifahari la Vicky Kamata linalifunika lile la bosi wake ambaye ni spika wa bunge, mheshimiwa Anne Makinda. Yeye nyumba yake ipo Kijitonyama.

ULINZI NYUMBANI KWAKE USIPIME
Uwazi lilipata bahati ya kufika nyumbani kwa Vicky  na kukumbana na ulinzi wa mitambo ya kisasa ya kuzuia wezi na majambazi kwa saa 24.
Ili mgeni aingie ndani ya geti huhojiwa na walinzi kwa dakika zisizopungua kumi.

WABAYA WAKE WAMUUNDIA ZENGWE LA FREEMASON
Huwezi kupendwa na kila mtu, hii ni baada ya mwandishi wa gazeti hili kuamua kupiga kambi kwa muda wa siku mbili jirani na nyumba ya mheshimiwa huyo ambapo baadhi ya watu waliohojiwa kuhusu ukwasi wa mbunge huyo mwanamke walisema huenda ni memba wa Freemason.

“Mafanikio ya mbunge huyu bwana ni makubwa mno, tunasikia watu wakisema huenda ni Freemason. Lakini ndivyo tulivyo Watanzania, mtu akifanikiwa kidogo wanasema ni Freemason, ninavyomfahamu huyu dada amepiga hatua, sijawahi kumsikia na mambo ya Freemason,” alisema jirani mmoja na kuungwa mkono na wenzake.
MSIKILIZE VICKY
Katika mahojiano maalum na Uwazi kuhusu utajiri wake, Vicky alisema:
“Mafanikio yote yametokana na juhudi zangu za kujituma katika kufanya kazi, namwamini Mungu siku zote. Hakuna dhambi mbaya hapa duniani kama kukata tamaa.

“Tukifanya kazi kwa kujituma na kumwamini Mungu hakuna Mtanzania maskini.
“Kila mtu ana uwezo wa kubadilisha mfumo wa maisha akiamua, umaskini wa watu si chaguo la Mungu, kila jambo litokealo kwa mwanadamu lina maana kubwa kwa Mungu.”

KAULI YA UWAZI
Wanawake nchini waige mfano wa Vicky kwa kukamata fursa mbalimbali na wanapofanikiwa wawasaidie wengine, kama kusomesha yatima na wasiojiweza

MWANAFUNZI WA CHUO AJINYONGA BAADA YA KUFELI MITIHANI

Mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Chuo cha Ualimu  cha Winneba, nchini Ghana, amejiua kwa kujinyonga mara baada ya jina lake kubandikwa kwenye ubao wa matangazo (notice board) kuwa amefeli masomo matatu.



Jina la mwanafunzi huyo limehifadhiwa kwa sasa, ila inasemwa kuwa sababu ya kujinyoga kwake ni kutokana na kufeli masomo hayo matatu ambapo kungepelekea kufutwa kwake shule hapo.

Sababu hasa ya kifo chake haijajulikana moja kwa moja ila inaaminika ilitokana na hofu ya kutimuliwa chuoni hapo kutokana na kufeli mitihani mitatu.

Wilson Dabuo, ambaye ni muwakilishi wa wanafunzi kwenye baraza la chuo hicho, alieleza kupitia Joy News kwamba chuo hicho kina sheria ya kutimua wanafunzi wanaofeli masomo matatu kwenye mitihani yao.

HATARI POSHO ZA SERIKALINI: WAJUMBE WA BUNGE LA KATIBA KUVUNA MILIONI 21...TSH 300,000/ KWA SIKU

HATIMAYE serikali imeweka hadharani kwamba kila mjumbe katika Bunge la Katiba ataweka kibindoni posho ya sh 300,000 kwa siku.


Kwa maana hiyo, kila mjumbe katika Bunge hilo atakuwa amelipwa sh milioni 21 kwa siku 70 za uhai wa Bunge hilo, na kama serikali itaongeza siku 20 zaidi kwa mujibu wa katiba na kufikia siku 90, kila mjumbe atavuna sh milioni 27.


Awali gazeti hili liliwahi kuripoti majadiliano ya ndani serikalini kabla ya jana kuthibitishwa rasmi ambapo kulikuwa na pendekezo la kutaka kila mjumbe alipwe sh 700,000 kwa siku.

Akizungumza na waandishi wa habari jana mjini Dodoma, Katibu wa Bunge Dk. Thomas Kashililah, alisema kuwa kila mjumbe katika Bunge hilo atalipwa sh 300,000 kwa siku.

Alisema malipo ya wajumbe hao ni pamoja na posho zote za vikao ikiwa imeunganishwa na posho za madereva.

Pia alieleza kuwa gharama zote ambazo zimetumika katika matengenezo ya ukumbi na sehemu nyingine ni sh bilioni 8.2 na fedha hizo ni bajeti ya kawaida ambayo ilipitishwa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2013/14.

Mbali na hilo, Kashililah alisema kuwa kutokana na umuhimu wa kuwepo kwa Bunge Maalumu la Katiba, Bunge limehakikisha linafanya ukarabati ikiwa ni pamoja na kufunga mitambo mbalimbali ya usalama na kurekebisha mifumo ya kiutendaji.

Alisema matengenezo yaliyofanyika ni pamoja na kurekebisha paa la jengo la ukumbi wa Bunge ambalo awali lilikuwa likivuja wakati wa mvua.

Akitoa ufafanuzi zaidi katika ufungaji wa viti ndani ya ukumbi wa Bunge hilo, alisema  kuna viti 678 na kurekebisha vipaza sauti ambapo kazi hiyo pekee imegharimu dola za Kimarekani milioni moja.

Kuhusu maandalizi, alisema yamekamilika na wajumbe wameishaanza kufika bungeni kwa ajili ya usajili.

Alisema vikao vya Bunge vitaanza  rasmi Februari 18 majira ya saa nane mchana na wataanza kwa kumchagua mwenyekiti na makanu wake.

Alisema ratiba ya Bunge la Katiba itaanza na mkutano wa maelekezo kwa wajumbe Februari 18 asubuhi na Bunge lenyewe litaanza siku hiyo hiyo saa nane mchana.

Kwa mujibu wa katibu huyo, shughuli nyingine zitakazofanyika ni pamoja na mwenyekiti wa muda kusimamia uandaaji  na upitishwaji wa kanuni.
Alisema mwenyekiti wa muda atasimamia uchaguzi wa mwenyekiti na baada ya kupatikana mwenyekiti na makamu wake, ndipo atakapopatikana katibu ambao wataapishwa na Rais Jakaya Kikwete.
Uhai wa Bunge hilo utakoma Aprili 30 au kwa ridhaa ya rais.
-Tanzania Daima

 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari