Like Us On Facebook
Showing posts with label Jackline Wolper. Show all posts
Showing posts with label Jackline Wolper. Show all posts

KIVAZI CHA AJABU CHA JACKLINE WOLPER CHAZUA GUMZO JIJINI DAR,KITAZAME MWENYEWE KIVAZI HICHO

Mastaa bongo movie walibaki hoi;wolper huu mwendo wake ni noumaaa...amekua gumzo sana katika Skukuu ya Krismas jinsi alivyo pendeza yani kama alicia keys vile..mtazame hapa pichani....



WOLPER NDANI YA BIFU ZITO NA ZAMARADI.SOMA KISA HAPA

Staa wa sinema za Bongo, Jacqueline Wolper amemrushia maneno ya lawama Mtangazaji wa Kipindi cha Take One, Zamaradi Mketema kuwa ni mnafki na adui yake mkubwa katika maisha.
Zamaradi Mketema.
Akizungumza , Wolper alisema amegundua kuwa mtangazaji huyo amekuwa akimfuatilia kwa karibu sana maisha yake kwa mtindo wa chanya (negative), akamuomba amuache.
Nilibadili dini kutoka Ukristo kwenda Uislamu, Zamaradi akanifuatilia, juzijuzi nimerudi kundini (kwenye Ukristo) kwa kusikiliza maneno ya wazazi wangu, akanifuatilia tena.
Huko nyuma kupitia kipindi chake alikubali nidhalilishwe na waigizaji wenzangu kwa faida yake (hakutaka kufafanua), iliniuma sana. Leo (hivi karibuni)  kaniweka hewani (kwenye redio) bila ya ridhaa yangu. Naomba niseme kuwa naanza kugundua azma yake kwangu ni nini, aniache na maisha yangu,” alilalama Wolper.
Baada ya Wolper kulalamika sana,  lilimtafuta Zamaradi kwa njia ya simu ya kiganjani ambapo alisema yeye anawajibika kwa kazi yake hakuna ishu ya kumfuatilia mtu.
 
“Mimi simfuatilii maisha yake, ni kazi tu. Kama mwandishi wa habari nikipata habari ya mtu natakiwa kubalansi (uwiano) naye,” alisema Zamaradi.


JACQUELINE WOLPER AKANA MADAI YA KUMPIGA KIBUTI DALLAS BAADA YA KUFULIA

Staa wa filamu Bongo, Jacqueline Wolper amefunguka kuwa suala la yeye kuachana na aliyekuwa mpenzi wake, Abdallah Mtoro ‘Dallas’ halikusababishwa na ukata kwani yeye hakufuata fedha kwa mwanaume huyo.
Akijibu swali la paparazi wetu lililomtaka afunguke kama alifuata mkwanja kwa Dallas, Wolper alisema moyo wake huwa hauna tamaa ya fedha na aliingia katika penzi la Dallas kwa mapenzi aliyokuwa nayo wakati huo na kwa kuwa yaliisha, maisha yanaendelea.
 
Sikufuata pesa kwa Dallas, pesa ni pesa na mapenzi ni mapenzi. Kama ni pesa nilikuwa nazo na hata kabla sijawa naye na sasa pia ninazo, waniache,” alisema Wolper.

HATIMAE JACKLINE WOLPER AFUNGUKA BAADA YA KUBADILI DINI KWA MARA YA PILI


Hatimaye mwanadada Jacqueline Wolper ameamua kuweka wazi kilichotokea mpaka kuamua kubadili Dini yake ya Uislamu na kurudi kwenye ukristo tena. Kupitia ukurasa wake wa mtandao mmoja wa kijamii mwanadada huyu wa bongo movies ametoa ujumbe ufuatao kwa mashabiki wake.

“…mambo mashabiki zangu.sikua na njia nyingne yakulikwepa hili nanaamini kua kwa wale mashabk zangu waislam amtomaind maana akuna mtu wakumsikiliza chin ya hanga zaidi yawazazi so imenipasa kurudi kanisani kwakauli yawazazi wangu.naamin kama aujaolewa ata uwe na miaka mingap bado unatakiwa kua chin ya imaya ya wazazi ata ukifa ujue unazikwaje na mimi ni binadam sijui saa wala dakika.muhm nikuwajuza nakuwaelewesha mashabk zangu stak maswal nawapenda wote…”

Hapo awali iliripotiwa kuwa mwanadada huyu ameamua kuwa mkristo tena baada ya penzi lake lililosababisha abadili dini na kuwa muislamu na jamaa aitwaye 'Dallas' kuvunjika hivi karibuni.

Swali ni je, atabadili dini tena akitokea mwingine wa dini aliyo tofauti na sasa?

Baada ya ndoa yake KUBUMA, Jack Wolper autema uislamu na kuurudia Ukristo

STAA anayefanya vyema katika tasnia ya filamu za Kibongo, 
Jacqueline Wolper ameamua kurudi katika imani yake ya awali ya Kikristo ikiwa ni miezi michache tangu alipotangaza kubadili dini na kuwa Muislamu. 
 

Wolper akiwa katika Kanisa la KKKT lililopo Kijitonyama wakati wa ibada.
 
Novemba 3, mwaka huu (Jumapili iliyopita) mwandishi wetu alimnasa Wolper katika Kanisa la KKKT lililopo Kijitonyama jijini Dar, akisali sambamba na waumini wa kanisa hilo.
 

Waumini wakiendelea na ibada ndani ya kanisa alimokutwa Wolper.
 
Bila ya kificho, Wolper ambaye alipokuwa Muislamu alikuwa akitumia jina la Ilham alisimama na kujitambulisha kama muumini mpya wakati mchungaji wa kanisa hilo alipowataka waumini wapya kufanya hivyo.

Wolper akiwa katika ibada kanisani hapo.
 
Wakati ibada hiyo ikiendelea, Wolper alionekana kuimba pambio kwa hisia kali na ibada ilipoisha, alitoka kanisani huku mkononi mwake akiwa ameshika Biblia.
 

Wolper (kulia) akiwa na muumini mwenzake nje ya kanisa.
Nje ya kanisa hilo, Wolper alionekana akiongea na wazee wa kanisa pamoja na baadhi ya waumini ambapo wote walimkaribisha kwa furaha.
 

Jacqueline Wolper akiwa katika vazi la Kiislamu wakati wa mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan mwaka jana.
 
Mwandishi wetu alimfuata Wolper na kumuuliza kilichomfanya arudi kwenye dini yake ya awali, naye alisema kwamba amefanya hivyo kutokana na msukumo wa wazazi wake ambao kwa muda mrefu walikuwa wakipinga kitendo chake cha kuwa Muislamu.
 
“Nimeamua kuurudia Ukristo kwa kuwa wazazi wangu kwa muda mrefu walikataa mimi kuwa Muislamu, kwa hiyo kuanzia sasa siyo Ilham tena, niite Jacqueline kama zamani,” alisema Wolper.

Wolper akiwa ndani ya gari aina ya BMW X6 alilonunuliwa na Abdallah Mtoro ‘Dallas’ baada ya kubadili dini na kuwa muislamu.
 
Mwaka jana, Wolper alibadili dini na kuwa Muislamu kutokana na kuwa na uhusiano na Abdallah Mtoro ‘Dallas’.
 
Dallas akiwa nje ya nchi akamtaka Wolper kubadili dini ili akirudi wafunge ndoa ya Kiislamu, Wolper alikubali na kufanya hivyo katika Msikiti wa Kichangani uliopo Magomeni jijini Dar na kuchagua jina la Ilham.
 
Gari aina ya BMW X6 alilonunuliwa Wolper na Dallas baada ya kuwa muislamu.
 
Dallas alirudi nchini lakini wawili hao  hawakufunga ndoa bali penzi lao likaingia doa na kumwagana, Wolper akaendelea na msimamo wa imani yake hiyo mpya na mara kwa mara alikuwa akidai kwamba hataiacha dini hiyo pamoja na kumwagana na Dallas.
---GPL

GONJWA LILE LA HATARI LAZIDI KUMTESA JACKLINE WOLPER


            Msanii wa filami nchini  maarufu  kwa  jina  la  Jackline Wolper  mwishoni  mwa  wiki  alijikuta  hoi  kitandani  ambapo  alilazimika  kukimbizwa  hospitali  huku  akiwa  hajitambui....

Mrembo  huyo  ambaye  amejizolea  sifa  nyingi  kutokana  na  filamu  zake  alikuwa  akisumbuliwa  na Malaria, gonjwa  hatari ambalo  limekuwa  likimsumbua  mara  kwa  mara...

Wolper  aliripoti  taarifa  ya   kuumwa  kwake  katika  account  yake  ya  facebook  na  kuweka  wazi kuwa  gonjwa  linalomsumbua  ni  lile  lile   hatari la  Maralia  ambalo  limekuwa  likimsumbua  mara  nyingi...

Kumbukumbu  zinaonyesha  kwamba,  mwaka  2010  aliwahi   kuugua  gonjwa  hilo  na  kulazwa  kisha  akapona.

MFAHAMU JACKLINE WOLPER FEKI ANAEWATAPELI WATU KWENYE MITANDAO YA JAMII


                    kumekuwa na wimbi kubwa la matapeli kwenye mitandao ya kijamii hususan FACEBOOK, TWITTER, BBM na mingine mingi. Jana katika pita pita zangu kwenye mtanfao wa Facebook nilipokea ujumbe ukionesha Jackline Wolper anaomba urafiki nami bila kusita nika confirm obi lake. Leo nilipoingia inbox yangu ya facebook nilikuta ujumbe huu.

Conversation started today


1:26am
Jackline Wolper
Hello, sorry naweza kukusumbua kitu nw?


3:04am
Pablo Junior Calter I
yeah sure.


3:14am
Jackline Wolper
Naomba nisaidie, niko nyumban and sijatoka bado kuna kaz naifanya kwenye computer, kazi ya ofisini. Umeme Umeniishia naomba niazime 20,000 ninunue then baadae nikitoka nakurudishia.

3:17am
Pablo Junior Calter I
ohky haina tatizo sasa hizo pesa nitakupatiaje ama una tigopesa?

3:29am
Jackline Wolper
0712394346, Jina litokee jackline massawe

3:31am
Pablo Junior Calter I
sawa wng so utanirudishia lini

3:36am
Jackline Wolper
Baadae nakutumia, kuna kazi nikiimaliza ndo ntatoka, naomba nitumie bas sasa ivi Pablo

3:52am
Pablo Junior Calter I
poa nakutumia
na hii ni picha ya chat tuliyofanya




chat yangu na jackline wolper feki

Facebook wapo watu wengi sana wenye hii tabia ambayo sio nzuri kwakweli wasanii wetu kila siku wana lalamika kuwa majina yao yanatumiwa vibaya jambo ambalo sio jema guys kwa wewe mwenye huu mchezo nakushauri uache maana iko siku utagundulika tu "ZA MWIZI NI AROBAINI".

fungua hapa kuangalia hio account fake ya Jackline Wolper

JACKLINE WOLPER HALI MBAYA HOSPITALINI...ASEMA "WATANZANIA NIOMBEENI...."

 
            Msanii wa Filam Tanzania ajulikanae kwa jina la Wolper yuko hoi Hospitalini huku akiomba Dua kwa wapenzi wake wamuombee ili apone haraka. Wolper ameripot taarifa za kuumwa kwake katika akaunti yake ya facebook na kuainisha ugonjwa unaomsumbua ni Maralia na ujumbe huo umesomeka hivi:

clip_image002

WOLPER ANASWA AKITWANGA MBEGE


          MWANADADA anayefanya vizuri kwenye tasnia ya filamu za Kibongo, Jacqueline Wolper Massawe ‘Gambe’ ameamua kudumisha mila na desturi baada ya kupiga picha akiwa anakunywa pombe ya kienyeji aina ya mbege.
Wolper alitundika picha hiyo katika mtandao wa Kijamii wa Instagram akiwa ameshikilia kikombe maarufu kinachotumiwa na watu wa Kilimanjaro kwa ajili ya kunywea pombe aina hiyo na kuambatanisha na maneno kuwa anadumisha mila.
“Nyumbani Arusha nikinywa wine nitakosea jamani, leo mbege tu Wachaga mtanielewa tu,”aliandika Wolper.
Baada ya kuweka picha na maneno hayo watu mbalimbali walionekana kumfagilia staa huyo na kumsifu kwamba ameonesha kujali mila tofauti na watu wengine pindi wanapokuwa mastaa huzibeza mila zao.
Mashabiki wengi walikuwa wakimpongeza kwa kumuandikia maneno kwa lugha ya Kichaga kuonesha kwamba wamemkubali.

WOLPER AWAPA USHAURI WA BURE WASANII WANAOVAA NUSU UCHI



Muigizaji wa filamu za  kibongo  maarufu  kwa  jina  Jackline Wolper amewaasa waigizaji wenzake wa kike kuacha kuvaa nguo za nusu uchi kwani ni kinyume na mila na tamaduni za kitanzania .

Wolper aliyasema hayo kufuatia kupigiwa kura na kushinda kama muigizaji wa kike mwenye muonekano wa kistaa...

Akizungumza katika kipindi cha filamu cha Take One kinachorushwa Clouds Tv , Wolper alisemakuwa  yeye hawezi kuvaa mavazi ya nusu uchi ila anavaa  mavazi yanayomsitiri mwili wake na bado anapendeza kuliko hao wanaovaa nusu uchi halafu hawapendezi.

"Nawashukuru  sana mashabiki wangu kwa kunipigia kura hadi kuibuka mshindi, na ni kweli najiamini kwa kuwa mimi hata siku moja huwezi kuniona nimevaa nguo za nusu uchi kama wengine" Wolper

WOLPER AVUNJA GLASI YA DIAMOND



           

                       STAA wa Bongo Movie, Jacqueline Wolper juzikati alijikuta kwenye wakati mgumu baada ya kuvunja glasi ya Rais wa Wasafi, Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Tukio hilo lilijiri Agosti 28, mwaka huu ndani ya Ukumbi wa Hoteli ya Serena, Posta jijini Dar ambapo staa huyo alikuwa kwenye uzinduzi wa video ya Diamond.
Ilikuwa wakati Diamond akisalimiana na mastaa mbalimbali, alipofika kwa Wolper aliigusa kidogo, ikaanguka.
Paparazi wetu alipomuuliza Wolper sababu ya glasi hiyo kuvunjika, alijibu: “Hata mimi sijui nini kimetokea, tulikuwa tunasalimiana ghafla tu glasi yake ikadondoka na kupasuka, sijui ni miujiza au nini loh!”
Diamond naye akatia neno: “Nimeshtukia glasi ipo chini tu, daah! Sina hata cha kueleza juu ya hili.”

-GPL

MPASUO WA WOLPER WACHANGANYA MIDUME

GAUNI alilolivaa mwigizaji wa filamu za Kibongo, Jacquline Wolper limeonekana kutibua hali ya hewa kutokana na ukubwa wa mpasuo kiasi cha midume kumtolea macho ya matamanio staa huyo.Tukio hilo lilichukua nafasi nje ya hoteli ya Serena iliyopo jijini Dar wakati wa utambulisho wa video ya staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul  ‘Diamond’ inayokwenda kwa jina la My number One.
 Wolper akiwa ameweka mapozi kwa ajili ya kupiga picha, aliwashtua wanaume waliokuwa wakielekea katika magari yao sehemu ya maegesho na kuanza kumtolea macho.

 “Father cheki mpasuo huo kushoto kwako hapo ulipokaa ni mahali pake?” alisikika mwanaume mmoja aliyepita karibu na alipokuwa amesimama Wolper.
Baada ya kusikika kauli hiyo, mwigizaji huyo alibaki akicheka na kusema kuwa hashawishiki na maneno yao.
“ Kwani ni peke yangu niliyevaa gauni lenye mpasuo mkubwa?” alihoji Wolper.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari