Like Us On Facebook

PICHA ZA FLORA MVUNGI AKIJIFUNGUA(AKIWA LEBA ZAVUJA)

               PICHA za mwigizaji Flora Mvungi (Hadija) ambaye ni mke wa msanii Hamis Baba ‘H. Baba’ akijifungua mtoto wa kike baada ya kusota kwa muda mrefu ZIMEVUJA

 Flora Mvungi (Hadija) akijifungua.
Kutoka kwa vyanzo vyake, mbali na picha za mtoto, Mwandishi wetu alilibamba tukio la Flora akijifungua Jumatano iliyopita katika Hospitali ya Marie Stopes iliyopo Sinza, Dar.

Flora akiwa hospitali na mumewe H. Baba.
Kwa mujibu wa H. Baba, alifurahishwa kuitwa baba kwani ni kitu ambacho alikuwa anatamani kwa muda mrefu na Mungu amemtimizia hivyo anamshukuru kwani ni zawadi kubwa katika maisha yake.

Mtoto wa Flora Mvungi.
Kwa upande wa Flora alikuwa na haya ya kusema: “Namshukuru sana Mungu kwa sababu niko salama na mwanangu, ukweli mwacheni mama aitwe mama kwani kuzaa siyo kazi rahisi”.
 
H. Baba alimalizia kwa kusema kuwa kama walivyosema awali kabla mtoto huyo hajazaliwa kuwa jina lake ataitwa Tanzanite, ndiyo hivyo itakavyokuwa jina hilo ndilo litakalotumika.
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari