Jambo limezua jambo! Mvua zilizonyesha na kusababisha mafuriko maeneo
ya Dumila mkoani hapa, zimemuumbua mke wa mtu ambaye jina lake
halikupatikana, akiwa anasaliti ndoa gesti.
Mafuriko hayo yalisababishwa na mvua kubwa zilizoanza kunyesha Jumatano iliyopita na kusababisha maafa makubwa yakiwamo kuharibiwa kwa makazi ya watu, majengo ya serikali zikiwamo shule, vyuo na mahakama.
Mafuriko hayo yalisababishwa na mvua kubwa zilizoanza kunyesha Jumatano iliyopita na kusababisha maafa makubwa yakiwamo kuharibiwa kwa makazi ya watu, majengo ya serikali zikiwamo shule, vyuo na mahakama.
“Umechelewa kidogo tu ungepata picha zao yeye na mke huyo wa mtu
wakipiga mbizi uchi wa mnyama wakitokea gesti, sijui jana usiku walilewa
sana mpaka wamechelewa kuamka na kukutwa na mafuriko, muda huu wa saa
nne asubuhi!”
Aidha, juzi Alhamisi, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Waziri wa Ujenzi,
John Magufuli walifika eneo hilo la tukio na kujionea hali halisi.
Akizungumza na wananachi wa Kijiji cha Magole, Pinda aliwaambia
serikali imetoa chakula kwa waathirika wa tukio hilo na kuwataka wanachi
kuwa wavumilivu katika kipindi hicho kigumu walichopitia.