Sosi huyo alizidi kutiririka na sentensi kuwa, kutokana na kipigo hicho, Aunty Lulu aliumia na kuanza kuvuja damu kisha akakimbizwa hospitali kwa Dokta Mvungi (Kinondoni) ambapo aliambiwa mimba imeharibika na kulazimika kusafishwa kizazi.
“Vikao vya kumsema mwanaume huyo kwa kosa alilofanya vilifanyika nyumbani kwao Jumapili ambapo aliahidi kutorudia tena na kuomba radhi huku akiahidi kumfanyia makubwa Lulu,” alisema sosi huyo makini.
Baada ya paparazi wetu kuzinyaka habari hizo, alimwendea hewani Aunty Lulu, alijibu kwa unyonge na kusema ndoto zake za kuwa na mtoto zimeyeyuka kufuatia kipigo hicho.
“Sina la kusema zaidi, ndoto za kuwa na mtoto zimeyeyuka mwanaume huyu amezidi wivu lakini sina jinsi kwa sababu ndio baba mtoto na ameshaomba msamaha,” alisema Lulu.
-GPL