Like Us On Facebook

ANT LULU AIBIWA NGUO ZA NDANI...ATOA ONYO KWA KURIPOTI KWA MGANGA WAKE BAGAMOYO


MSANII wa filamu za Kibongo aliyeibukia kwenye utangazaji, Lulu Semagongo ‘Aunty Lulu’ amekombwa vitu kibao vya thamani dukani kwake na watu wasiojulikana.

Tukio hilo la kuhuzunisha lilitokea wiki iliyopita, usiku wa manane katika duka la msanii huyo lililopo  Kinondoni – Biafra jijini Dar es Salaam ambapo vitu vilivyoibwa ni pamoja na Chupi zake,  viatu, nguo, pochi, simu na fedha.

“Kwa kweli nimechanganyikiwa sana, hadi sasa bado sijajua thamani ya vitu vyote kwa jumla ni kiasi gani lakini nasema sitaki lawama. Walioniibia ni heri wanirudishie tu kwa njia yoyote maana kitakachowakuta hawatasahau.

“Nimeshakwenda Bagamoyo kwa mtaalamu wangu na kazi imeshakwisha. Natoa siku saba vitu vyangu viwe vimerudi vinginevyo...” alisema Aunty Lulu bila kufafanua zaidi.


TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari