“Mimi ni Mlokole na nampenda Mungu kuliko watu wanavyofikiria, nimeshasikia maneno yakidai nimeachana na wokovu, lakini hawajui suala la wokovu ni la mtu binafsi na Mungu wake,” alisema Dokii.
Alisema jamii isipende kuingiza tamaduni za nchi na dini, kwani katika nchi dini zilikoanzia hayo ni mambo ya kawaida na ndiyo imani yao inavyowaambia.