Like Us On Facebook

CLOUD 112 ATOA SABABU ZA MAINDA KUPOTEA....

                                                    Cloud 112

MKALI wa sinema za Kibongo, Mussa Issa ‘Cloud 112’ amemchana mwigizaji Ruth Suka ‘Mainda’ kuwa stori nyingi za filamu nchini haziendani na Mainda na kudai ndiyo sababu za staa huyo kupotea. 
 Ruth Suka ‘Mainda’.
Akipiga stori na paparazi wetu, Cloud 112 alisema maprodyuza wanashindwa kumchezesha Mainda katika ngazi muhimu kama ya mke kwani stori zinakuwa zinahitaji watu wenye umbo kubwa.
“Stori nyingi zinamkataa Mainda, mfano mimi siwezi kuigiza naye kama mke na mume kwani umbile lake na langu haliendani hivyo natoa wito kwa wasanii kumsaidia Mainda sababu ana uwezo mkubwa wa kuigiza,” alisema Cloud 112.

Source: GPL
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari