Like Us On Facebook

WASTARA ATOA SIRI ZA SHIJA KUMTAKA ILA AKAZIDIWA KETE

 Mwanadada Wastara ametoa siri ambayo alikuwa hajawahi kuizungumza katika maisha yake ya uhusiano, kisa hicho kinachofurahisha kinahusu maisha yake na marehemu mume wake na sababu iliyomfanya afunge naye ndoa.



"Unajua Shija domo lake lilikuwa zege kumbe alikuwa ananitaka lakini akashindwa kuongea hadi mwenzake Sajuki (marehemu mumewe) alipotuma maombi na kusikilizwa, Baada ya Sajuki kukamilisha kila kitu na kuwa mke na mume ndiyo aliponitonya  kuhusu habari ya Shija kuwa wakati wananifuata kumbe alikuwa ananitaka ila marehemu Sajuki akawa mjanja." alisema Wastara

Shija mwenyewe anasema kuwa wakati huo alipokuwa anamtaka Wastara yeye alikuwa makini na kazi hasa utayarishaji wa filamu na suala la mapenzi lilikuwa la ziada.


TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari