Wema Sepetu.
Akichati na Ijumaa juzi kupitia mtandao wa Instagram Wema alisema:
“Siwezi kusema niko na furaha kabisa. Nimesema niondoke zangu Bongo
kimyakimya kuja huku kuhangaikia kazi zangu, nimeonekana nimekuja kuuza
unga.“Maskini ya Mungu naishi maisha yangu wala sina habari na mtu, sijawahi hata siku moja kufikiria kufanya biashara hiyo, leo nimelia na naumia sana.”
Madai ya Wema kunaswa China kwa soo la ‘poda’ yamekuja ikiwa ni siku chache tu tangu Video Queen, Rehema Fabian akiri kutupwa selo nchini humo kwa kesi ya madawa ya kulevya.
-GPL