Like Us On Facebook

HIVI NDIVYO MWENYEKITI WA CCM MKOA WA MWANZA ALIVYOUWAWA NA WANANCHI KWA KUPIGWA MAWE.


Aliyekuwa mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza ndugu Clement  Mabina  ameuwawa na wananchi wenye hasira kali kwa kupigwa mawe huko maeneo ya Kisesa jijini Mwanza...
  
 Chanzo cha kuuwawa ni kwamba mabina aliwanyang'anya ardhi wananchi hao na kesi ikawa mahakamani na leo mchana Mabina bila kibali cha mahakama alikuwa anapanda miti na kujenga msingi wa nyumba ndipo wanachi wakaenda kumhoji iwaje anapanda miti na kuweka msingi kwenye viwanja hivyo ilhali kesi ipo mahakamani?...
  
 Mabina alianza kutoa lugha chafu na kurusha risasi hovyo  ambapo  alifanikiwa  kumuua  mwananchi  mmoja. Baada  ya  mauaji  hayo, wananchi  nao  walichachamaa  na  kujikuta  wakimuua  kwa  kumpiga  mawe

TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari