Like Us On Facebook
Showing posts with label Matukio. Show all posts
Showing posts with label Matukio. Show all posts

WANASAYANSI WADAI MWISHO WA DUNIA UTAFIKA BAADA YA MIAKA BILIONI 3.5 AMBAPO JUA LITAKUWA KALI SANAA



             Mwisho wa dunia kwa mujibu wa wanasayansi bado sana. Maisha duniani yataendelea kuwepo kwa miaka bilioni 3.5 mingine.

Baada ya hapo wanasayansi wanaamini jua litakuwa kali kiasi ambacho hakuna kiumbe kitakachoweza kuishi. Tangu iwepo, sayari ya dunia imekuwa kwenye umbali sahihi kutoka kwenye jua kiasi cha kuifanya iwe  na maisha.

Wanasema tatizo ni kwamba nyota zimeendelea kuchemka kadri muda unavyoenda na zikiendelea kutoa joto zaidi, maji ya dunia yataendelea kukauka na kupote kabisa. 

Utabiri huo umetoka kwa wataalam wa chuo kikuu cha East Anglia ambapo mtafiti mmoja wapo, Andrew Rushby amesema baada ya miaka hiyo dunia itakuwe na joto kali kiasi ambapo hata bahari zitageuka kuwa mvuke.
 
Alisema binadamu watakuwa viumbe wa kwanza kupotea.

Source: Daily Mail via Bongo5

TAZAMA PICHA TISA ZA MWANAMKE MWENYE KUCHA NDEFU KULIKO WOTE DUNIANI.

kucha-6              Walton ambaye pia ni mwanamuziki alihudhuria uzinduzi wa Guinness World Records 2014 uliofanyika London, Uingereza Jumanne wiki hii.

kucha-1
kucha-2
kucha-4
kucha-5
kucha-7
kucha-8
kucha-3
kucha-9

Bongo5

MATUKIO KATIKA PICHA WAKATI WA MAZISHI YA ASKOFU KULOLA HAPO JANA JIJINI MWANZA.



 Mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo akiongoza wanachi kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Askofu wa EAGT Moses, Kulola 



























Mchungaji Kadani Limbu ambaye ni Katibu wa Kanisa la EAGT Makao Makuu (Ujenzi) akisoma wasifu wa marehemu Askofu Kulola aliyezaliwa 1928 katika Kijiji cha Nyang’honge Wilayani Kwimba Mkoani Mwanza na kujaliwa kupata elimu ya msingi (Middle School) na sekondari ya Bwiru Boys Mwanza kati ya mwaka 1946 hadi 1949 kuendelea na masomo na kupata Civil Technician.

Baada ya kumaliza na kupata utaalamu huo na kuajiliwa kuwa mtumishi wa serikali katika Halmashauri ya Mji wa Mwanza kama Mhandisi wa Mchoraji wa Ramani za majengo na Barabara wakati wa uhai wake aliamua kuacha kazi na kuanza utumishi wa mungu akifanya kazi kwa kutembea kila mahali akihubiri Injili kwa watu mbalimbali.

Wasifu huo ulimwelezea Askofu Kulola wakati wa utumishi wake wa kiroho kuwa  alikuwa akitembea kwa miguu kuanzia mwaka 1962 akihubiri neno la Mungu .Baada ya kuacha kazi za serikali mwaka 1951 alipatwa na matatizo na kuwahi kufungwa gerezani na kupigwa na bwana jela na kuumizwa vibaya muguu wake wa kushoto na kupelekea kupata kilema ambapo aliwekewa mguu wa bandia.

Marehemu Askofu Kulola ameacha mke na watoto 10 wajukuu 42 vitukuu 16 na amekuwa mutumishi wa kiroho tangu  akiwa na umri wa miaka 18 ....
-Gsengo

TAARIFA KAMILI YA JESHI LA POLISI KUHUSU BOMU KATIKA KANISA LA KKKT DAR ES SALAAAM...

POLISI Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, imebaini kuwa chombo kilichodhaniwa kuwa bomu katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kijitonyama hakikuwa bomu, bali ni kifaa cha Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) cha kuchunguza anga.


Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleman Kova alisema hayo jana alipozungumza na waandishi wa habari, baada ya kufanya uchunguzi kwa kushirikiana TMA.
"Baada ya kupata taarifa, polisi walifika eneo la tukio na kukuta kifaa kilicho katika umbo la kasha kikining'inia kwenye transfoma karibu na Kanisa kikiwa kinawaka taa.
“Katika kasha hilo kulikuwa na maandishi ya kalamu ya wino yaliyosomeka TMA na Airport," alisema Kamanda Kova.


Alisema baada ya uchunguzi wa awali, polisi walibaini kuwa kifaa hicho si bomu na kuondoka nacho kwa uchunguzi zaidi. Mtabiri Mwandimizi wa hali ya hewa kutoka TMA, Augustino Kanemba, alisema kifaa hicho kinaitwa Radio Sound na hutumiwa na Mamlaka hiyo kufanya utafiti wa hali ya anga za juu.


"Kifaa hiki hurushwa juu kuleta taarifa ya hali ya anga, kwa kawaida hufungwa puto ili kipae angani na baada ya kufika juu, puto hupasuka na kutua sehemu yoyote ya Dar es Salaam … hili si bomu," alisisitiza Kanemba.


Hata hivyo, Kamanda Kova alipongeza washarika wa Kanisa hilo, kwa kutoa taarifa Polisi na kuomba waendelee kufanya hivyo wanapoona kitu wasichokielewa.
Akizungumzia mlipuko katika Kanisa la KKKT, Usharika wa Segerea, Kamanda Kova alisema Polisi Kanda Maalumu Dar es Salaam, kwa kushirikiana na wataalamu wa fani za ugaidi na matumizi ya mabomu kutoka makao makuu ya Jeshi hilo, wanafanya upelelezi kubaini waliohusika na tukio hilo.


Katika tukio hilo la Agosti 24 mwaka huu saa 8 usiku, waumini wapatao 20 wakiwa wanaendelea na ibada, ghafla walitokea watu wanne na kuingia kanisani na kutupa chupa ya bia ikiwa na utambi na mafuta yadhaniwayo kuwa ya taa eneo la madhabau na kusababisha mlipuko.
Katika hatua nyingine, Polisi imekamata wahalifu 180 wakiwamo majambazi katika msako ulioendeshwa na Jeshi hilo ndani ya wiki moja. Pia imekamata bastola mbili, risasi tisa, magunia mawili ya bangi na magari mawili ya wizi.

SOURCE: HABARI LEO

HUYU NDIE NYOKA MKUBWA MWENYE MIGUU ALIYEGUNDULIKA CHINA


 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari