WACHEZAJI wa Manchester United waliamua
kujifariji na mwanzo mbaya wa msimu wa timu yao kwa kuhudhuria onyesho
la rapa Jay-Z jana.
Wilfried Zaha, Danny Welbeck, Ashley Young na Patrice Evra walipigwa picha wakitoka kwenye onyesho hilo.
Welbeck - akitoka kufunga bao katika
Ligi ya Mabingwa dhidi ya Shakhtar Donetsk katikati ya wiki- alikuwa
mwenye furaha na tofauti na wenzake watatu baada ya shoo hiyo ya Hip
hop.
Furaha kama Ashley? Danny Welbeck akiwa
mwenye tabasamu pana, wakati Ashley Young akiwa ameinamisha kichwa chini
wakati wanaondoka
Niangalie! Shabiki mmoja mwenye furaha alipigwa picha karibu na Patrice Evra, wkati Wilfried Zaha akiondoka kinyonge
Mtu mzima ndani ya nyumba: Nyota wa United walikuwa Manchester kuangalia shoo ya Jay-Z
Kikosi cha David Moyes kitasafiri
Sunderland kwa ajili ya mechi ya Jumamosi, kikiwa na matarajio ya
kizunduka baada ya kufungwa mechi tatu kati ya nne za Ligi Kuu England.
Wako chini mno kwenye msimamo, nafasi ya
12 wakizidiwa pointi nane na vinara Arsenal na wazi wanahitaji pointi
Uwanja wa Light kujiweka sawa.
Chini na juu: David Moyes amekuwa katika mwanzo mgumu ndani ya miezi yake miwili ya awali kama kocha wa United
Hoi: United ilifungwa nyumbani na West Brom ikitoka kufungwa na Manchester City wiki moja kabla
Lakini kufuatia sare ya Ukraine, bila shaka United wataingia na moto mkali dhidi ya Black Cats.
Wakati huo huo, Ryan Giggs amesema wachezaji ndio wanaostahili lawama kwa mwanzo mbaya na si Moyes.
Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 39-
amejitolea kumtetea bosi wake, akisema: "Siwezi kumnyooshea mtu kidole
kwa haya yanayotokea. Hatujacheza vizuri inayostahili wote kama
wachezaji binafsi na hata kama timu,"alisema.
kazi nzuri: Welbeck aliifungia United bao la kusawazisha katikati ya wiki Ligi ya Mabingwa
"Tunafahamu ubora katika chumba cha
kuvalia nguo. Sisi ni mabingwa, hivyo tulionyesha ubora mwaka jana na
tunatakiwa kuonyesha tena,".
"Sir Alex alikuwa kocha babu kubwa na
mwenye nguvu kubwa katika klabu. Utamkumbuka mtu kama huyo. Lakini
sifikiri kwamba inaweza kuwa sababu wakati wachezaji hawachezi vizuri
kibinafsi kama wanayotakiwa.
"Hatuchezi vizuri kama timu. Hatujapata tatizo la majeruhi kama tulilokuwa nalo kipindi kilichopita- hakuna kisingizio,"alisema.