Like Us On Facebook

VURUGU ZATOKEA MOMBASA BAADA YA MAUAJI YA MASHEIKH, KANISA LACHOMWA MOTO

             Sheikh Ibrahim Omar aliuawa kwa kupigwa risasi akiwa na washirika wake watatu. 
Salvation Army Church


Polisi ya Kenya imetangaza kuwa, watu wanne akiwemo Sheikh Ibrahim Ismail Rogo wameuawa baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana ndani ya gari dogo jana usiku huko mjini Mombasa.



Taarifa ya Polisi  ya Kenya imeeleza,  Sheikh Ibrahim Rogo alikuwa mrithi wa Sheikh Aboud Rogo ambaye  naye aliuawa na familia yake kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana mwezi Agosti 2012. 



Mauaji ya Sheikh Ibrahim Rogo ambayo yameutikisa mji wa Mombasa, yametokea  baada ya kupita takriban wiki mbili tokea kundi la al Shabab lilipovamia  na kuua  watu wasiopungua 63 na kujeruhi mamia ya wengine kwenye jengo la maduka ya biashara la Westgate jijini Nairobi. 
Baadhi ya wananchi wa Mombasa wanakituhumu kikosi  maalumu cha kupambana na ugaidi kuwa ndicho kilichotekeleza  mauaji hayo. 
Sheikh Ibrahim Rogo ambaye alikuwa akitoa mihadhara kwenye Msikiti wa Musa mjini Mombasa alituhumiwa na jeshi la polisi kuwa anawachochea vijana wa Kiislamu kujitumbukiza kwenye makundi  ya kigaidi.
 Polisi ya Kenya imesema kuwa, Gaddafi Mohammad, Issa Abdallah  na Omar Abu Rumeisa ni miongoni mwa waliouawa, naye Salim Aboud alinusurika kwenye shambulio hilo.

Salvation Army Church

TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari