Sheikh Ibrahim Omar aliuawa kwa kupigwa risasi akiwa na washirika wake watatu.
Salvation Army Church |
Polisi
ya Kenya imetangaza kuwa, watu wanne akiwemo Sheikh Ibrahim Ismail Rogo
wameuawa baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana ndani ya gari
dogo jana usiku huko mjini Mombasa.
Taarifa ya
Polisi ya Kenya imeeleza, Sheikh Ibrahim Rogo alikuwa mrithi wa Sheikh
Aboud Rogo ambaye naye aliuawa na familia yake kwa kupigwa risasi na
watu wasiojulikana mwezi Agosti 2012.
Mauaji
ya Sheikh Ibrahim Rogo ambayo yameutikisa mji wa Mombasa, yametokea
baada ya kupita takriban wiki mbili tokea kundi la al Shabab lilipovamia
na kuua watu wasiopungua 63 na kujeruhi mamia ya wengine kwenye jengo
la maduka ya biashara la Westgate jijini Nairobi.
Baadhi ya wananchi wa Mombasa wanakituhumu kikosi maalumu cha kupambana na ugaidi kuwa ndicho kilichotekeleza mauaji hayo.
Sheikh
Ibrahim Rogo ambaye alikuwa akitoa mihadhara kwenye Msikiti wa Musa
mjini Mombasa alituhumiwa na jeshi la polisi kuwa anawachochea vijana wa
Kiislamu kujitumbukiza kwenye makundi ya kigaidi.
Polisi
ya Kenya imesema kuwa, Gaddafi Mohammad, Issa Abdallah na Omar Abu
Rumeisa ni miongoni mwa waliouawa, naye Salim Aboud alinusurika kwenye
shambulio hilo.
Salvation Army Church |