Like Us On Facebook

NYUMBA ANAYOISHI KIUNGO WA YANGA NIYONZIMA YATEKETEA KWA MOTO



                NYUMBA anayoishi kiungo wa Yanga SC, Haruna Niyonzima, maeneo ya Magomeni Makuti, Dar es Salaam imeungua moto usiku wa kuamkia leo na kusababisha hasara ya vitu kadhaa.  Habari zilizoifikia BIN ZUBEIRY zimesema kwamba nyumba hiyo anayopanga mchezaji huyo wa kimataifa wa Rwanda, imeungua zaidi eneo la sebuleni na fenicha zote, Teleisheni na Redio zimeteketea kwa moto.

Janga hilo lilitokea wakati mchezaji mwenyewe akiwa ndani ya nyumba yake na kama si jitihada za majirani kujitokeza kumsaidia kuzma moto huo, athari zingekuwa kubwa. Imeelezwa nyumba hiyo ina wapangaji wawili na upande ulioathirika kwa moto ni ambao anasihi mchezaji huyo tu. Jitihada za kumpata Haruna mwenyewe haraka kuzungumzia suala hilo hazijafanikiwa na zinadenelea, wakati Ofisa Habari wa Yanga SC, Baraka Kizuguto alisema amesikia taarifa hizo ila anasubiri kupata uhakika kamili kutoka kwa mchezaji mwenyewe.






















“Kweli ninawashukuru sana majirani kwa kuonyesha uungwana wa hali ya juu, bila ya wao nyumba yote ingeungua.
CREDIT : SALEH JEMBE
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari