MWAKA
 2005 nilikuwa nikipanda daladala na Naseeb Abdul (Diamond) katika kituo
 cha Shule Tandale Magharibi jijini Dar es Salaam. Wakati huo, sikuwa 
hata na wazo kwamba atakuja kuwa mtu maarufu katika muziki hata 
kushughulisha watu kutaka kujua zaidi kuhusu maisha yake. 

Baada ya hapo nikaanza kuona wimbo wake wa kwanza kwenye video, ‘Nenda Kamwambie’ kilikuwa kibao kizuri kilichompa umaarufu, ndipo alipoanza kunivutia kusikiliza nyimbo zake. Baada ya video ile sikumuona tena kituoni kama ada yetu, nikaanza kusikia anaendesha gari aina ya Toyota Celica.
Kutoka mwaka 2006 mpaka sasa ni mfululizo wa mafanikio aliyoendelea kuyapata kijana huyu aliyezaliwa Septemba 28, 1988 mpaka kuwa mwanamuziki wa kwanza Tanzania kulipwa pesa nyingi kutokana na shughuli hiyo.
Kutokana
 na utafiti uliofanywa na tovuti inayozungumzia masuala ya vijana 
inasemekena ‘Diamond Platnamz’ anapata kiasi cha Sh Mil 16 kwa matamasha
 mawili anayofanya katika mwezi.
Mbali ya mikataba minono aliyoingia na makampuni mbalimbali yanayonufaika kwa taswira ama sauti ya mwanamuziki huyo kijana, Diamond anaingiza fedha nyingi kila anaposafiri nje ya Tanzania na bara la Afrika kufanya matamasha ya muziki.
Mbali ya mikataba minono aliyoingia na makampuni mbalimbali yanayonufaika kwa taswira ama sauti ya mwanamuziki huyo kijana, Diamond anaingiza fedha nyingi kila anaposafiri nje ya Tanzania na bara la Afrika kufanya matamasha ya muziki.
 Wakati
 Diamond, ambaye hajatimiza hata miaka kumi kwenye tasnia ya muziki kuna
 mtu mmoja anaitwa Muhidini Gurumo, amejishughulisha na muziki kwa 
takriban miaka 45 lakini kila alipokutana na swali hili kutoka kwa 
wanahabari kuwa kwa kipindi chote hicho muziki umemsaidia nini, jibu 
lake ni: “Bado hakuna ninachoweza kujivunia kupitia muziki, hali ya 
maisha ni ngumu.”
 Gurumo
 ambaye alizaliwa 1940 alianza muziki mwaka 1959 akiwa na bendi ya 
Kilimanjaro Chacha Band. Sasa ni takriban miaka 45, umri wa baba mwenye 
wajukuu lakini alichofanikiwa ni kujenga nyumba mbili na kupata shamba 
moja. Gari lenyewe alizawadiwa na Diamond mwaka huu baada ya kulalamika 
sana kwenye vyombo vya habari.
 Nini Tatizo
 Maalim
 Gurumo (Kamanda), analalamika kuwa wanamuziki wa kizazi kipya 
wanasifiwa sana na vyombo vya habari. Akisisitiza kuwa hawana ubunifu, 
nyimbo zao hazina athari katika jamii na hudumu chini ya mwaka mmoja 
zinapoteza taswira.
 Lakini
 amesahau kuwa wanamuziki wa sasa wengi wamejiajiri, kipindi hicho bendi
 nyingi zilimilikiwa na kampuni, taasisi ama mtu ambaye anapenda sanaa 
hiyo ya muziki.
 Lakini sasa wanamuziki wameamka, wanajimiliki wenyewe pesa wanazopata zinaingia mifukoni mwao.
 Mathalan
 tangu Diamond aanze kuimba ameshaingia zaidi ya mikataba kumi tofauti 
ambayo ilimnufaisha yeye kama Diamond, matamasha yake yanamnufaisha 
yeye, kikundi anachomiliki anakilipa kiasi wanachokubaliana kutokana na 
uwezo wa mwanakikundi.
Mwaka
 jana, 2012, Diamond aliingia mkataba na kampuni ya I-View Studios wa 
kusimamia kazi zake zote kwa miaka miwili. Huu ni mkataba ambao 
umemjengea heshima kubwa sana. Ingawa kiasi cha malipo kilifanywa siri 
lakini inaonekana ni mkataba mnono.
 Kampuni
 nyingine ya One Touch, ilifunga naye mkataba wa kuwa wasemaji wake. 
Yaani kila anachotaka kufanya ama kuzungumza kwenye jamii, ikiwa kuna 
kampuni inataka kufanya naye mazungumzo ya kibiashara, One Touch Company
 ndio watakaofanya kazi hiyo.
 Hilo
 tu linamfanya Diamond awe na uwezo mkubwa wa kupata fedha kutokana na 
muziki. Mara nyingine msanii anashindwa kujua thamani yake, anaweza 
kutaja kiasi kidogo cha fedha katika ‘dili’ kubwa. Lakini kwa kupata mtu
 wa kukusimamia kwenye mazungumzo ya kifedha lazima uwe tajiri.
 Aidha,
 bendi ambazo Maalim Gurumo amehama kutokana na sababu za kimaslahi 
hazipungui kumi, alianza na Kilimanjaro Chacha Band, Kilwa Jazz Band, 
NUTA Jazz Band, Mlimani Park, Safari Sound Ochestra, Rufiji Jazz, na 
nyingine nyingi kabla ya kumalizia muziki kwenye bendi kongwe ya Msondo 
Ngoma Music Band.
 Kote
 huko alizunguka kwa kutumia kichwa kitupu kujadili thamani ya sauti 
yake, hakuwa na mshauri wa masuala ya muziki ambaye atamwambia kutokana 
na thamani yako usikubali kuhama bendi hii ili kuenda bendi nyingine 
bila kupewa kiasi fulani cha fedha.
 Aliweza
 kuitwa baa akawa anakunywa bia na nyama choma huku anajadili 
mustakabali wa maisha yake na mkurugenzi wa bendi pinzani na anayofanyia
 kazi.
 Katika
 mazungumzo yake na wanahabari Maalim Gurumo aliwahi kutamka kuwa 
anatamani siku zirudi nyuma ili anufaike na muziki wake. Lakini nakataa,
 hata awe vipi kutokana na mfumo anaoutumia hawezi kuwa tajiri kama 
Diamond.
 Leo
 hii, Maalim Gurumo akiandaa tamasha na kuingiza Sh Mil 50, basi 
atakachoambulia ni asilimia  10 ya mapato ambayo ni Sh Mil 5, ambacho 
kitakuwa ni kiasi kikubwa kuwahi kukipata kwa tamasha moja tangu aanze 
kuimba.
 Lakini
 siku hiyohiyo Diamond akialikwa katika tamasha hilo la Gurumo ataondoka
 na Sh Mil 8 taslimu bila kupungua senti. Bado tofauti ipo kubwa.
 Aidha,
 mbali ya mapato ya stejini lakini Diamond ana mikataba minono na 
makampuni ya simu ambayo yanatumia nyimbo zake kama miito ya simu, ana 
mkataba mwingine mnono na kampuni ya Vodacom, ana mkataba na kampuni ya 
vinywaji baridi ya Coca Cola hata kufikia kujiita Coke Boy.
 Tukiwakusanya
 wanamuziki wa zamani kuanzia Mbaraka Mwinshehe mpaka kufikia Maalim 
Gurumo, bado hawawezi kufikia mafanikio ya muda mfupi aliyoyapata kijana
 mdogo Naseeb Abdul ‘Diamond’ ambaye hata ladha ya ndoa hajaionja 
kutokana na umri wake kuwa mdogo.
 Wakati
 Gurumo akijisifia nyumba mbili alizojenga kwa tamu, Diamond ana nyumba 
zaidi ya mbili ambapo moja amemjengea mama yake yenye thamani inayofikia
 zaidi ya Sh Mil 50.
 Pengine Gurumo ni mwanamuziki bora zaidi kuliko Diamond lakini mwenziye amemzidi kwenye ujanja wa kutafuta fedha
-muhariri wa gazeti la Raia  Mwema 

