Like Us On Facebook

JOHARI AAMUA KUJIFUNGIA NDANI BAADA YA FUMANIZI ILI KUKWEPA AIBU



               Muigizaji maarufu Blandina Chagula(Johari) anadaiwa kuishi kwa kujificha ficha baada ya hivi karibuni kumshushia makonde muigizaji mwenzake Chuchu Hans ambapo kisa kilidaiwa ni kugombea penzi la Vicent Kigosi(Ray). 

Inadaiwa Johari hataki hata kukutana na watu wake wa karibu wakiwemo wasanii wenzake. 

Chanzo kimoja kikizungumza na Globalpublishers kilisema  kuwa  kwa sasa Johari hataki kabisa kuonana na watu wake wa karibu, hata mtaani amekuwa haonekani mara kwa mara, anawakwepa hata wasanii wenzake, hii ni kutokana na lile sakata lake na Chuchu...

Nae Johari alipoulizwa na mtandao huo juu ya sababu ya kujifungia ndani alisema: "Niko nyumbani, sitaki kutembea sana kwani niko na likizo fupi, halafu hata hili sakata langu na Chuchu bado halijapoa"
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari