Like Us On Facebook

MKE WA SHEHE PONDA AZUA SIMANZI MAHAKAMANI

WAKATI Katibu wa Taasisi na Jumuiya za Kiislam Tanzania, Shehe Ponda Issa Ponda akiendelea kuhenyeka gerezani, mkewe Mariam Ponda, Agosti 27, mwaka huu alitia simanzi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Mkoa wa Morogoro na kusababisha watu kumuonea huruma.
                                                  Mke wa Sheikh Ponda, Mariam Ponda.
Mama huyo alitia simanzi hiyo wakati mumewe alipofikishwa mahakamani hapo kwa mara ya pili kwa ajili ya muendelezo wa kesi ya uchochezi inayomkabili.
Akiwa mahakamani hapo, baada ya mumewe kusomewa mashitaka matatu yanayomkabili na wanasheria wake, Bernard Kongola na Sunday Hyera  kukana, mwanamke huyo alikimbilia mlangoni ili kumsabahi kwa kushikana naye mikono lakini ilishindikana.
                                                        Sheikh Ponda akiwa kizimbani leo.
Ilimuuma sana, machozi yalimlenga machoni ambapo alilazimika kujifuta kwa baibui alilojitanda huku akiinamia chini kwa huzuni.
Hata hivyo, mwanamke huyo hakukata tamaa,  mumewe alipopandishwa kwenye gari la kumrudisha Segerea Dar, alilifuata na kutaka kumpa mkono lakini alizuiwa na maafande wa magereza waliokuwa wakimlinda, kitendo kilichomfanya ainame tena kwa huzuni.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba 11, mwaka huu na mtuhumiwa huyo amerudishwa gerezani
Source:GPL.
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari