Like Us On Facebook

BREAKING NEWS: WATU 13 WAMEFARIKI KATIKA AJALI YA GARI HUKO SHINYANGA...

Habari zilizoufikia mtandao huu hivi punde zinasema kuwa watu 13, wamefariki dunia na 11 wamejeruhiwa katika ajali mbaya iliyotokea usiku wa kuamkia leo katika kijiji cha ngongwa mkoani shinyanga kwenye ajali iliyohusisha gari aina ya hice lenye namba za usajiri t 756 chx na gari lililokuwa limeharibika lenye namba za usajili t 696 ams.

Akizungumza kwa njia ya simu kaimu kamanda wa polisi mkoa wa shinyanga, kihema kihema, alisema kuwa miongoni mwa watu waliofariki dunia ni pamoja na dereva wa hice, iliyokuwa na abiria hao ikitokea kahama kuelekea ushirombo ambaye alifariki papo hapo, huku majeruhi wakipelekwa kupatiwa huduma ya kwanza katika hospitali ya wilaya ya kahama.
  KILELE CHA HABARI tunatoa pole kwa wahanga wa ajali hiyo....
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari