Like Us On Facebook

MAMA KANUMBA ATEMBEZA BAKULI KUOMBA MSAADA BAADA YA MAMBO KUWA MAGUMU

MAMA wa msanii nguli wa filamu nchini marehemu ‘Steven Kanumba’ Frola Mtegoa amesema yuko katika mkakati wa kuandaa filamu inayohusu maisha ya mwanaye kiasi cha kufikia hatua ya kuomba msaada ‘kutembeza bakuli’.
 
Mama mzazi wa marehemu ‘Steven Kanumba’ Frola Mtegoa.
Akizungumza na paparazi wetu mama huyo alisema kwamba, anapata wakati mgumu kukamilisha jambo hilo kutokana na kukwama na kutaka asaidiwe ili kufanikisha jambo hilo.
“Nimekwama na nawaomba wadau wajitokeze kunisaidia nikamilishe hili, nahitaji msaada wa kifedha na hata ushauri,”alisema.
Mama huyo alisema lengo la kuandaa kazi hiyo ni kutaka kufikisha ujumbe katika jamii kwa kuamini kwamba wengi watajifunza kupitia maisha ya mwanawe.

 
Marehemu Steven Kanumba.
Amemtaka yeyote ambaye atakayeguswa na jambo hilo asisite kuwasaliana naye na kumsaidia.
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari