Like Us On Facebook

Huu Ndio Ujumbe wa Mshabiki wa Man Utd kutoka Bongo kwenda kwa Kocha David Moyes


Mpendwa Moyes,Kwa heshima na taadhima juu ya ukweli kwamba uliteuliwa na Sir Alex Ferguson, ningependa kutoa maoni namna nisivyoridhishwa na namna unavyoendelea kuharibu ngome ambayo ilituchukua miaka mingi kuijenga. Kwanza, kuhusu mchezo dhidi ya Everton, haikuwa siri kwamba  Fellaini, Giggs na Wellbeck hawakuwa na msaada kwa timu… huzuni ni kwamba Kagawa na Rafael wakawa wahanga wa ile  'small team mentality' ambayo inaonyesha wazi ni vigumu kuiondoa kichwani mwako!! Ukamuingiza Chicharito dakika za mwisho ili nae akumbane na aibu uliyotuletea. Ikiwa bado hujajua, wewe sasa ni kocha Manchehester United na utamaduni wa Manchester united hatuchezi ili kushinda tu mechi kadhaa bali ni kushinda ubingwa wa ligi. KUTOKA KWENYE MTAZAMO WA KIJAMII Je una ufahamu wowote namna ulivyotutengenezea mazingira magumu sisi mashabiki wa (MAN UTD) kuvaa jezi zetu za MAN UTD?? Unajua namna ambavyo tunaepukana na mitandao ya kijamii kwa kuogopa madongo na maneno ya kejeli ya wapinzani wetu? Nina uhakika ulisikia, wakati ukiwa Everton kwamba sisi tuna kelele na tunaongea sana kuhusu ubora wa yetu lakini mpaka sasa hautupi msingi wa kuweza kuizungumzia timu yetu kwa mazuri, unatupa unyonge ambao hatuujozea. MTAZAMO WA KIUCHUMI Jaribu kufikiria kuhusu wale wenzetu ambao huwekeza fedha zao katika michezo ya kubet ambao sasa wengine wanafilisika kutokana na timu kufanya vibaya.Angalia namna mapato ya baa na migahawa yanavyoathirika kwa sababu wengi wetu mashabiki wa United tunaangalia mpira tumejifungia majumbani mwetu. Nafahamu unajua wengi wetu tunakunywa sana. MTAZAMO WA KIIMANI. Vitabu vya dhambi zetu hivi sasa vimezidi kuisha kurasa kwa sababu umetufanya tumekuwa tunatukana sana siku hizi, kutabasamu kwetu imekuwa tatizo na badala yake presha zetu zinaishia kwa wake zetu, watoto wetu na watu wetu wa karibu wasio na hatia.MTAZAMO WA KIAFYA Maisha yetu ya siku hizi yamekuwa kama wagonjwa wa "Insomnia" (Ugonjwa wa ukosefu wa usingizi) wiki mpaka wiki, wengi wetu mashabiki wa Man UTD sasa tumekuwa katika hatari ya kupata magonjwa ya presha kwa msongo wa mawazo unaotupa, pia unajua madaktari wengi ni mashabiki wa Man UTD hivyo unaweza ku-imagine namna wagonjwa ambao ni mashabiki wa  Arsenal, Chelsea na Liverpool wanavyokuwa katika wakati mgumu kutibiwa vizuri (especially in the theatre)Nakataa kuamini kwamba sisi ni timu ndogo kwa sababu tumekuwa tukitafuna zetu bubble gum na kubeba tu makombe. Tumegoma kutumia mikono yetu yote miwili kuhesabu tofauti ya pointi zilizopo baina yetu na viongozi wa msimamo wa ligi. Tumegoma kuona ukiwaacha wachezaji wa maana kwenye benchi na kufanya majaribio yake na Fellaini(Nyoshi), Giggs na Welbeck.  Nakutakia kheri ukiwa unaanza vita ya kupigania ajira yako ndani ya old Trafford na ningependa kukushauri kwamba jaribu kutafuna bubble gum, utaonekana vizuri kiasi. P.S: Hongera kwa kutimiza lengo lako; Kuifunga Ma  UTD ndani ya old Trafford na kutibua rekodi yetu. Kwa huzuni kubwa na masikito,Ni mie mshabiki mkubwa  Man UTD 
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari