
Johannesburg/Dar.
Watanzania wawili wanahojiwa na Polisi wa Afrika Kusini baada ya kukamatwa jana na kilo 55 za dawa za kulevya.
Watu
 hao wawili wanatazamiwa kufikishwa mahakamani kesho kujibu tuhuma za 
kukamatwa na dawa hizo zenye thamani ya Rand75 milioni (Sh11.7 bilioni).
Maofisa
 wa Kikosi Maalumu cha Kupambana na Makosa ya Jinai na Rushwa cha Afrika
 Kusini (The Hawks), kiliwakamata watu hao katika Kitongoji cha Kempton 
Park, Ekurhuleni, Jimbo la Gauteng.
Msemaji
 wa Hawks, Paul Ramaloko alisema jana kuwa maofisa hao walivamia nyumba 
waliyokuwa wanaishi Watanzania hao na kukuta mzigo huo.
Hata
 hivyo, alikataa kutaja majina ya watu hao kwa kuhofia kuharibu 
uchunguzi akisema bado walikuwa wanawasaka watuhumiwa zaidi wakiwamo 
raia wa Afrika Kusini.
Alisema
 kikosi chao kimepata mafanikio makubwa kwa kukamata dawa nyingi kiasi 
hicho... “Tunakaribia kuwakamata vinara wa biashara hiyo, maana 
tumeelezwa kuna kundi kubwa la watu wazito,” alisema Ramaloko. Hii 
inakuwa mara ya pili katika kipindi cha miezi minne kwa Watanzania 
kutuhumiwa kubeba dawa hizo.
Julai
 mwaka huu, wasanii wawili Agness Gerald `Masogange’ na Melissa Edward 
walikamatwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Oliver Tambo, Johannesburg wakiwa 
na kilo 180 za kemikali aina ya ephedrine zenye thamani ya Sh7 bilioni.
Baada
 ya kukaa miezi miwili jela, Masogange alipatikana na hatia ya kuingiza 
kemikali hiyo, ambayo hutumika kutengeneza dawa za kulevya na kutozwa 
faini ya Rand 15,000 (Sh2.3 milioni).
Melissa aliachiwa huru baada ya kuonekana hana hatia.
Wasafirishaji sasa watumia samaki
Katika
 hatua nyingine, wasafirishaji wa dawa za kulevya inasemekana wamebuni 
mbinu mpya ya kutumia samaki kusafirisha bidhaa hiyo haramu.
Akizungumza
 jana wakati wa uteketezaji wa dawa za kulevya, Mkuu wa Kitengo cha 
Kudhibiti Dawa za Kulevya, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi 
(SACP), Godfrey Nzowa alisema wanatumia samaki kwa kuwa wana harufu 
kali.
-Mwananchi
-Mwananchi

