Like Us On Facebook

HUSNA IDDI AIONGELEA NDOA YA CHAZ BABA AMBAYE ZAMANI ALIKUWA MPENZ WAKE



               MWIGIZAJI wa sinema zao la Shindano la Kimwana Manywele, Husna Idd ‘Sajent’ amesema haumizwi kichwa na ndoa ya mzazi mwenzake, Charles Gabriel ‘Chaz Baba’ na mwanadada Janeth Sospeter.

Akiongea  na  GPL  jijini Dar es Salaam Sajent alisema kitendo cha mzazi mwenzake huyo kufunga pingu za maisha hivi karibuni hakimsumbui kabisa akili kwani anaamini hata yeye anaweza kumpata mtu na kufunga naye pingu za maisha muda si mrefu.



“Hilo la kufunga ndoa mimi wala halinitishi kwa vile matunzo ya mtoto ananipatia sina presha na ndoa yao, acha waishi kwa raha zao nami nakula bata kivyangu,” alisema Sajent.

TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari