Like Us On Facebook

RAY C: NAPAMBANA, NASHINDA MITIHANI

MWANAMUZIKI Rehema Chalamila ‘Ray C’ ambaye alikuwa hoi kwa madawa ya kulevya, juzikati ametupia maneno ya faraja kwenye mtandao wa Instagram akieleza kuwa amekuwa akipewa mitihani migumu katika maisha yake lakini kwa uwezo wake Mungu amekuwa akishinda.


Ray C anayetarajia kurejea kwenye ‘game’ hivi karibuni, akasema anaamini yeye ni msichana imara kutokana na namna alivyokuwa akipambana na sasa ni Ray C mpya.
Aliandika hivi: “The New Ray C, am strong lady (Ray C mpya, mimi ni msichana imara)…kila nipewapo mtihani mgumu wa maisha napigana mpaka nakuwa mshindi.”
Pia kupitia mtandao huo, Ray C alitupia video ambayo anasikika akiimba wimbo wa msanii wa THT,Winfrida Josephat ’Recho’ uitwao Upepo kisha akaandika: “I love your voice my sis.” Recho akajibu: Thanks a lot my dada.”
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari