Like Us On Facebook

CHALZ BABA AIFUNGUKIA NDOA YAKE!

         SIKU chache baada ya kuvuta jiko, Prezidaa wa Mashuja Band, Charles Gabriel ‘Chaz Baba’ amesema anafurahia maisha ya ndoa na kamwe kazi haiwezi kumtenganisha na mkewe.
 Akizungumza na paparazi wetu hivi karibuni, Chaz Baba alisema anamshukuru Mungu kwa kuwa mkewe, Rehema Sospeter ni muelewa hivyo atakapokuwa mzigoni usiku, hawezi kuwa na hofu.
“Mimi na mke wangu tumedumu kwenye uchumba kwa takriban miaka minne hivyo ananijua kiundani na mimi namjua pia, hatuwezi kutofautiana,” alisema Chaz. Mkali huyo alitarajiwa kurudi jukwaani Ijumaa hii (jana) baada ya kumalizika kwa fungate lake
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari