Like Us On Facebook

WANASAYANSI WADAI MWISHO WA DUNIA UTAFIKA BAADA YA MIAKA BILIONI 3.5 AMBAPO JUA LITAKUWA KALI SANAA



             Mwisho wa dunia kwa mujibu wa wanasayansi bado sana. Maisha duniani yataendelea kuwepo kwa miaka bilioni 3.5 mingine.

Baada ya hapo wanasayansi wanaamini jua litakuwa kali kiasi ambacho hakuna kiumbe kitakachoweza kuishi. Tangu iwepo, sayari ya dunia imekuwa kwenye umbali sahihi kutoka kwenye jua kiasi cha kuifanya iwe  na maisha.

Wanasema tatizo ni kwamba nyota zimeendelea kuchemka kadri muda unavyoenda na zikiendelea kutoa joto zaidi, maji ya dunia yataendelea kukauka na kupote kabisa. 

Utabiri huo umetoka kwa wataalam wa chuo kikuu cha East Anglia ambapo mtafiti mmoja wapo, Andrew Rushby amesema baada ya miaka hiyo dunia itakuwe na joto kali kiasi ambapo hata bahari zitageuka kuwa mvuke.
 
Alisema binadamu watakuwa viumbe wa kwanza kupotea.

Source: Daily Mail via Bongo5
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari