Like Us On Facebook

WEMA AFUNGA MWAKA KWAKUWEKA PICHA MTANDAONI IKIONYESHA UZURI WA MGONGO WAKE

Beautiful Onyinye wa Bongo, Wema Sepetu hivi karibuni ameachia picha tata kwenye akaunti yake ya Mtandao wa Instagram zikimuonesha akiwa ameacha mgongo wazi, jambo lililotafsiriwa na wengi kuwa ameamua kufunga mwaka huu kwa staili hiyo ya kuacha mgongo nje, Showbiz inakudondoshea.
Wema Sepetu akiwa ameacha mgongo wake wazi.
Katika picha hizo, Wema anaonekana kujichora tatoo kibao kuanzia shingoni na kumfanya aonekane tofauti na alivyozoeleka jambo lililofanya wengine wamsifie huku wengine wakimponda mbaya.
“Sasa Wema kujichora hivyo mgongoni ndiyo nini? Bora ungeuacha mgongo wako kama ulivyokuwa zamani,” alichangia mmoja wa wadau na kuungwa mkono na wenzake.
Showbiz ilipomvutia ‘waya’ Wema ili kumuuliza kulikoni ameamua kupiga picha za kuuanika mgongo wake, simu yake ilikuwa ikiita bila kupokelewa.
-GPL
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari