
Rais Jakaya Kikwete leo ametengua uteuzi wa mawaziri wanne kufuatia shutuma nzito dhidi yao katika sakata la Operesheni Tokomeza Ujangili.
Mawaziri waliopoteza ajira 
zao usiku huu ni pamoja na Khamis Kagasheki (Maliasili na Utalii), David
 Mathayo (Mifugo na Uvuvi), Emmanuel Nchimbi (Mambo ya Ndani) na Shamsi 
Vuai Nahodha (Ulinzi na JKT).
Akizungumza Bungeni Dodoma 
usiku huu, Waziri Mkuu Mizengo Pinda alikiri kulikuwa na matatizo 
makubwa katika usimamizi wa zoezi hilo.
“Tulifanya
 operesheni kwa nia nzuri,” alisema Waziri Mkuu Pinda  na  kuongeza : 
“Tatizo ni namna operesheni hiyo ilivyotekelezwa.”
  
Katika mdahalo uliogusa nyoyo
 za wabunge na wachambuzi mbalimbali wa siasa leo, wabunge waliueleza 
umma jinsi ambavyo Operesheni hiyo ilitumika kutesa, kunyanyasa na kuua 
raia wasio na hatia na kuwadhulumu mali zao.


 
 
 
 
 
 
