Like Us On Facebook

ANTI LULU ATUNDIKWA MIMBA

MSANII wa filamu, Lulu Semagongo ‘Anti Lulu’ baada ya kurukaruka sana, sasa inadaiwa ni mjamzito wa takribani miezi mitano.
 
Lulu Semagongo ‘Anti Lulu’.
Akilinyetishia Ijumaa juu ya ishu hiyo, rafiki wa karibu wa Anti Lulu aliyeomba hifadhi ya jina lake alisema, msanii huyo sasa amekuwa mtumiaji mzuri wa maembe mabichi huku magauni mapana yakiwa ndiyo mavazi yake.
“Mwanzo alikuwa anaficha lakini sasa siyo siri na mwenyewe ameona ni bora kuwataarifu ndugu na marafiki zake,” alisema mtoa habari huyo.
Katika kujua undani wa hilo, waandishi wetu walimsaka Anti Lulu na kufanikiwa kumuona akiwa na kitumbo chake lakini akaomba asipigwe picha ila akasema: “Mmechelewa kujua, mbona inakwenda mwezi wa tano sasa, mwenye mzigo mtamjua nikishajifungua jamani,”alisema msanii huyo.
-GPL
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari