Like Us On Facebook

DR WA MAREHEMU MICHAEL JACKSON AFUNGUKA MAMBO MAZITO KUHUSU MAREHEMU BAADA TU YA KUACHIWA HURU TOKA GEREZANI

Kwenye mahojiano yake ya kwanza mara baada ya kuachiwa toka gerezani kwa kuhusishwa na kifo cha nguli wa muziki wa pop duniani Michael Jackson, Dokta Conrad Murray alielezea kwenye mahojiano aliyofanya na The Mail kwamba, Michael hakuwa baba wa hata mtoto wake mmoja, aliathiriwa na madawa kiasi cha kufikia hatua ya kuhitajika kuwa anavaa condom sababu mkojo ulikuwa unatoka wenyewe kwenye uume wake.

“Unataka kufahamu ni kwa kiasi gani mimi na Michael kwa vile tulikuwa karibu? Nilikuwa nikishukilia uume wake kila usiku. Nilikuwa namvalisha condom sababu mkojo wake ulikuwa ukitoka wenyewe. Michael alikuwa hajua namna ya kuvaa condom, hivyo ilinibidi niwe namvallisha. Kilikuwa ni kitu cha kipekee sana ila aliniamini mimi. Sikumuuwa Michael Jackson, aliathiriwa na madawa, Michael Jackson kwa bahati mbaya alimuuwa Michael Jackson, naamini aliamka na kuamua kufanya aliyozoea kufanya, akajidunga sindano haraka ambayo ilisababisha kumpeleka kwenye hali iliyomfika.’’ 

Alikuwa kwenye majanga mwishoni mwa maisha yake, akiwa na msongo wa kimawazo na kupaniki … Mwishoni, Michael alikuwa mtu aliyekata tamaa. Nilijaribu kumlinda ila mwisho wa siku niliangushwa naye.

Jackson alikuwa ameingia kwenye matatizo ya kuathirika kiakili na kimwili kutokana na ziara yake ya London.’’ Alisema Dokta Conrad Murray.
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari