Like Us On Facebook

VIDEO: WATU WATATU WANAOSADIKIWA KUWA NI MAJAMBAZI WAUAWA JIJINI DAR ES SALAAM


                Watu watatu wanaosadikiwa kuwa majambazi wakiwa na silaha za moto wameuwawa na wananchi wenye hasira kali baada ya watu hao kujaribu kuwakimbia askari polisi katika mtaa wa sikukuu- Ilala jijini Dar es salaam.  
Kamanda wa polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam Suleimani Konda amesema majambazi hao walikuwa na silaha moja aina ya Smg na risasi 6 na baada ya kugundua  kufuatiliwa na polisi walifyatua risasi kujihami ambapo mbali na watu hao kuuwawa na wananchi jeshi hilo linamshikilia mtu mmoja aliyeokolewa na polisi katika mapigano hayo akiwa na hali mbaya na amelazwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili chini ya ulinzi mkali wa polisi kwa mahojiano zaidi.
 
Aidha kamishna Kova amebaini kufuatia msako mkali unaofanywa na jeshi la polisi katika jiji la Dar es Salaam wamefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 113 kwa makosa mbalimbali,silaha za moto 6,sare za jeshi, cd mbili zenye mafunzo ya kigaidi pamoja na magari mawili ya wizi ambapo amesema msako huo bado unaendelea ili kumaliza kabisa matukio ya uhalifu hapa nchini
.
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari