Like Us On Facebook

"SITASAHAU KAMWE JINA ALILOKUWA AKINIITA BABA...." WEMA SEPETU

Wema Isaac Sepetu ‘Madam’

WEMA Isaac Sepetu ‘Madam’ amefunguka kuwa kamwe hatasahau jina la Miss World ambalo marehemu baba yake, mzee Isaac Abraham Sepetu alikuwa akimuita.
Akizungumza na mwanahabari wetu wakati wa kuaga mwili wa baba yake nyumbani kwao, Sinza-Mori jijini Dar, Jumanne iliyopita, Wema alisema baba yake alikuwa akimuita jina hilo kama utani kutokana na masuala ya urembo aliyokuwa akiyafanya hivyo alipofariki dunia jina hilo ndiyo kumbukumbu yake ya muhimu.
Marehemu Isaac Abraham Sepetu.
“Sitalisahau jina la Miss World, baba ndiye alikuwa akiniita hivyo kila nilipokutana naye. Aliponiita hivyo nilikuwa nikifurahi sana,” alisema Madam.
Mwili wa baba Wema ulisafirishwa Jumatano (jana) kuelekea visiwani Zanzibar kwa ajili ya mazishi.

TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari