Like Us On Facebook

POCHI YA MKONONI YAFICHA MTOTO MCHANGA

Pochi
                                 Pochi ni ya kuwekea hela..
Polisi nchini Marekani wanamshikilia mama mmoja baada ya kukuta ameficha mtoto mchanga ndani ya pochi yake.
Polisi katika visiwa vya Virgin wamesema walikuwa katika ukaguzi wa kawaida barabarani na kumsimamisha mwanamama huyo majira ya saa tatu na robo asubuhi siku ya Jumanne.
Mtandao wa cnews.com umesema afisa wa polisi alimsimamisha mwanamke mmoja na kutaka kuona leseni yake lakini mara akasikia sauti ya mtoto akilia.
Polisi huyo hakuweza kumuona mtoto lakini akawa akiendelea kusikia sauti ya mtoto, na hivyo kumuuliza mama huyo yuko wapi mtoto anayelia.
Polisi wamesema mama huyo alifungua zipu ya pochi yake na kumtoa mtoto mchanga wa kike.
Mwanamama huyo amesema alijifungua mtoto huyo wiki moja iliyopita akiwa nyumbani kwake.
Mtoto huyo amepelekwa hospitali na mama huyo huenda akakabiliwa na mashtaka ya uhalifu kwa kutompeleka hospitali mwanaye, baada ya kujifungua.
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari