
Hit maker wa Roho yangu, Rich Mavoko amesema ameanza kupata mafanikio makubwa katika muziki wake baada ya kununua gari aina ya Nissan pamoja nyumba ambayo bado anaendelea kuijenga mkoani Morogoro.
Nyumba ya Rich Mavoko ambayo ipo Morogoro “Sina cha kusema muziki unalipa, nyumba yangu ni kubwa sana na pia nimejaribu kuonyesha ni mafanikio gani ambayo nimeyapata mpaka sasa. Kwahiyo namshukuru Mungu na mashabiki ambao wananiwezesha,” amesema Mavoko.
Gari ya Rich Mavoko.
“Wapo ambao walipata bahati kama yangu
wakashindwa kuitumia, kwa mimi nimetumia nafasi niliyoipata, ndio maana
nafanya mambo makubwa kama ninavyoingia gharama ya laki 8 kwajili ya
mavazi kwenye shoo zangu kubwa. Kila show kubwa natoa laki 8 kwa mbunifu
wangu.”
Aliongeza kuwa muziki hauna bahati bali ni kujituma.
