Like Us On Facebook

BINTI ALIYEACHISHWA KAZI KWA KITENDO CHA KUJIREKODI VIDEO AKICHEZA AKIWA OFISINI APATA AJIRA

             Kitendo cha msichana aliyeacha kazi kwa kujirekodi video akicheza muziki ofisini majira ya saa 10 alfajiri na kuipost youtube kama njia ya kumfikishia boss wake ujumbe wa kuacha kazi, hatimaye kimezaa matunda baada ya video hiyo kutazamwa na mamilioni ya watu akiwemo star Queen Latifah ambaye ameamua kumpa kazi.
Queen Latifah akiwa na msichana wa ‘I Quit’ Marina kwenye kipindi chake

Msichana huyo aitwaye Marina Shifrin ‘I quit girl’ aliyekuwa mfanyakazi wa kampuni ya Kikorea iitwayo Next Media Animation amegeuka kuwa staa kwenye internet kwa mzaha huo alioamua kuufanya wiki iliyopita, wa kujirekodi akicheza wimbo wa Kanye West ‘Gone’, huku maneno ya sababu za kuacha kwake kazi yakipita. Video hiyo mpaka sasa imetazamwa mara 13,999,571.


Baada ya Queen Latifah ambaye ana reality show yake ya TV inayoitwa jina lake kuitazama video hiyo alimkaribisha katika kipindi chake baada ya kuitazama video hiyo, na kuamua kumpa ajira Marina katika kipindi chake kwa cheo cha “Digital Content Producer”. Latifa alimwambia msichana huyo kuwa anapenda kufanya kazi na watu watulivu, wabunifu na wanaofurahisha sifa ambazo yeye anazo. Tazama Video ya Queen Latifah akiwa na Marina katika kipindi chake

Tazama video ya Marina iliyompa kazi kwa Latifa
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari