Like Us On Facebook

AFARIKI BAADA YA KUKOSA HEWA BAADA YA TANKI LA MAFUTA KULIPUKA



          ITV imeshuhudia jitihada za jeshi la polisi na kikosi cha zimamoto na uokoaji wakishirikiana na wananchi katika kuondoa mwili wa marehemu ambapo wakizungumzia tukio hilo baadhi ya mashuhuda wamesema  marehemu alikuwa akichomelea vyuma ndani ya tenki hilo lililokuwa limeharibika ambapo gafla ulitokea mlipuko na kupelekea marehemu kukosa hewa ingawa  jitihada za kumtoa akiwa Hai zilishindikana kutokana na kukosa hewa.

Kwa upande wake mwakilishi wa zamu wa kikosi cha zimamoto na uokoaji mkoa wa Morogoro Masoud Ramadhan amesema uchunguzi wa haraka uliofanyika umebaini  kuwa baada ya kutokea mlipuko uliosababishwa  harufu kali ya mafuta ndani ya tank hilo na ambapo mamehemu alikosa hewa

Mwili wa marehemu umechukuliwa na jeshi la polisi na kuhifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya mkoa wa Morogoro

TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari