Like Us On Facebook

HAKIMU ACHOMWA KISU MAHAKAMANI WAKATI AKITOA HUKUMU HUKO SHINYANGA

 
            Hakimu wa mahakama ya Mwanzo mjini Shinyanga Mheshimwa Nyanguoa Masaba amejeruhiwa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali akiwa Mahakani akitoa  hukumu.

Tukio hilo limetokea leo katika mahakama ya mwanzo mjini Shinyanga.

Hakimu huyo alijeruhiwa na mlalamikaji katika kesi ya wizi wa Baiskeli wakati akitoa hukumu.

Tukio hilo limesababisha mahakama hiyo kusimama kumnusuru hakimu huyo na kumkimbiza katika hosptali ya Mkoa kwa matibabu.

Mtuhumiwa wa tukio hilo Emmanule Zenge naye alijeruhiwa kwa kipigo na kupelekwa katika hosptali ya Mkoa.

Jeshi la polisi mkoani shinyanga limethibitisha kutokea kwa tukio hilo.


Star Tv
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari