Like Us On Facebook

WAKAMATWA WAKIWA NA MAITI YENYE MADAWA YA KULEVYA



            Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kamishna wa polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam Suleimani Kova amesema ugunduzi huo ulibainika baada ya uchunguzi uliofanywa na madaktari wa hospitali ya taifa Muhimbili wakishuhudiwa na polisi pamoja na baadhi na ndugu wa marehemu ambapo ameelezea marehemu alikutwa na hati za dharura za kusafiria nchi za nje na kuwa uchunguzi zaidi unafanyika kubaini mtandao mzima wa usafirishaji wa dawa hizo uliomuhusisha marehemu. 
 
Katika tukio lingine kamanda Kova amesema jeshi hilo linamshikilia mtu mmoja aliyejifanya kuwa mtumishi wa wizara ya afya na ustawi wa jamii aliyekamatwa katika hospitali ya taifa Muhimbili akiwa amevalia mavazi ya kidaktari pamoja na nyara mbalimbali zenye nembo ya hospitali hiyo kwa lengo la kuwaibia watu.
 
Kutokana na tukio la ugaidi nchini Kenya kamanda Kova amesema jeshi hilo limejipanga kuimarisha ulizi maeneo yote yenye mkusanyiko wa watu wengi na kutoa wito kwa jamii kuendelea kutoa taarifa kwa jeshi la polisi pindi watakapo baini mtu au kikundi cha watu wanaowatilia shaka.
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari