BAO pekee la Dejan Lovren limeipa Southampton ushindi wa 1-0 Uwanja wa Anfield dhidi ya wenyeji Liverpool leo.
Mwanasoka huyo wa kimataifa wa Croatia alifunga bao hilo dakika ya 54 na kumaliza rekodi ya Liverpool kutofungwa ndani ya mechi 12.
Mshambuliaji Luis Suarez, alikuwepo jukwaani akishuhudia mechi yake hiyo ya mwisho katika adhabu ya kufungiwa mechi 10 na sasa anarejea uwanjani.
Pamoja na hayo The Saints, inabidi wamshukuru refa Neil Swarbrick aliyewanyima Liverpool penalti baada ya beki wao kumuangusha Daniel Sturridge kwenye eneo la hari kipindi cha kwanza.
Kikosi cha Liverpool kilikuwa: Mignolet, Toure, Skrtel/Alberto dk72, Agger/Enrique dk56, Sakho, Gerrard, Lucas, Henderson, Aspas/Sterling dk46, Moses na Sturridge.
Southampton: Boruc, Clyne, Lovren/Fonte, Shaw, Wanyama, Schneiderlin, Rodriguez/Cork dk89, Lallana/Ward-Prowse dk75, Osvaldo, Lambert/Davis dk61.

Bao la ushindi: Dejan Lovren amfunga bao pekee la ushindi dhidi ya Liverpool

Amepatia: Wachezaji wa Liverpool wakiangalia mpira uliopigwa kwa kichwa na Lovren ukitinga nyavuni

Babu kubwa: Lovren akishangilia mbele ya mashabiki wa Southampton

Amekosa: Daniel Sturridge aisikitika baada ya kupoteza nafasi ya kufunga


Hasira: Brendan Rodgers na Steven Gerrard wakionyesha hasira zao za kufungwa

Kifaa: Victor Moses akiichezea Liverpool kwa mara ya kwanza Uwanja wa Anfield

Jino kwa jino: Kolo Toure na James Rodriguez wakigombea mpira

Mkwaju: Steven Gerrard akipiga mpira wa adhabu

Vita: Mamadou Sakho na Nathaniel Clyne wakigombea mpira

Anatazama: Luis Suarez akiangalia mechi Anfield

Mchuano: Adam Lallana akipambana na Steven Gerrard
-DARAJANI
KIUNGO John Obi Mikel amefunga bao lake la kwanza katika Ligi Kuu ya England na kuiwezesha Chelsea kuibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya Fulham Uwanja wa Stamford Bridge, huo ukiwa ushindi wao wa kwanza mwezi huu.
Mabao ya Oscar na Mikel kipindi cha pili yamemaliza ukame wa ushindi ndani ya mechi nne na kuendeleza rekodi ya Jose Mourinho kutofungwa nyumbani katika Ligi Kuu ndani ya mechi 63 na ushndi wa kwanza tangu wafungwe na Aston Villa.
Ushindi huo wa 2-0 unamaanisha Fulham inatimiza miaka 34 bila kushinda Stamford Bridge, Chelsea ikizinduka baada ya vipigo vya Everton na Basle.
Kikosi cha Chelsea kilikuwa: Cech, Ivanovic, Cahill, Terry, Cole, Ramires, Mikel, Schurrle/Lampard dk79, Oscar, Hazard/De Bruyne dk85, Eto’o/Torres dk64.
Fulham: Stockdale, Riether, Amorebieta, Hangeland, Richardson, Duff/Taarabt dk64, Parker, Sidwell, Kacaniklic/Tue Na Bangna dk72, Kasami/Rodallega dk85 na Bent.

Ushindi umerudi: Oscar akishangilia bao lake na wenzake

Oscar amefunga bao la kwanza leo Stamford Bridge

Bao tamu sana: John Obi Mikel akifunga bao lake la kwanza Ligi Kuu England baada ya mechi 258

Raha sana: Obi akishangilia bao lake

Raha zimerejea Darajani: Jose Mourinho akishangilia ushindi wake wa kwanza mwezi huu

Mwenye timu tabasamu latosha: Roman Abramovich akiwa jukwaani kuangalia ushindi wa timu yake

Amekosa: Darren Bent alipoteza nafasi nzuri ya kufunga wakati timu hizo hazijafungana

Maumivu: Scott Parker akichezewa rafu na Gary Cahill

Hdi chini: Steve Sidwell akimuacha chini Eden Hazard baada ya kugombea naye mpira

Mabao wapi?: Samuel Eto'o kwa mara nyingine ameshindwa kuifungia timu yake mpya

John Terry akiwania mpira wa juu

Branislav Ivanovic akipambana na Pajtim Kasami

Ramires, akipambana na Alexander Kacaniklic