Like Us On Facebook

BINTI AMKATAA MWANAE BAADA YA KUMZAA KISA HANA UWEZO WA KUMLEA

Ni katoto ka kike kenye afya teleee na ana siku tatu tu toka kuzaliwa.Bahati mbaya amezaliwa katika mazingira ambayo mama yake hayupo tayari kumlea na ilikuwa amtupe wasamaria wema wakaokoa jahazi.
Mama wa mtoto ndio huyu pichani anadai hana wazazi walifariki.Akawa analelewa na dada yake huko Sinza na akapata ujauzito.Baada ya kupata ujauzito dada akamfukuza nyumbani na aliyempa ujauzito akamkataa.
Kina mama pichani wakimwogesha mtoto baada ya kuzuia zoezi la mama kutupa mtoto
Inavyosemekana mama wa mtoto alienda dispensary kuchoma sindano mimba itoke.Bahati nzuri mtoto siku zilikuwa zimetimia akamzaa.Alipozaliwa na kuwa hai mama mtoto akawa hamtaki anataka kumtupa.Mama wa mtoto hamtaki kabisaaaa mwanae.
Kina mama baada ya kuzima zoezi la mtoto kutupwa wakakaa na binti kuelewa nini kinamsibu.Wakamuogesha mtoto na mama yake pia akaogeshwa.Akapewa maneno ya kumsaidia kisaikolojia lakini haikusaidia mama msimamo wake ukawa ule ule.Mama aliyekuwa akimuogesha mtoto yupo radhi kumchukua mtoto na kumlea kama wa kwake maana mama yake hamtaki.

Niliwahi kuona movie zamani inafanania na hili binti mdogo alipata ujauzito lakini hakuwa tayari kuwa mama na akamtoa mwanae kwa mtu na mkewe waliokuwa wanamatatizo ya kupata mtoto.Alimtoa kwasababu yeye asingeweza kulea na kumpa mahitaji yote.Yule baba na mkewe ndio walikuwa wakihitaji mtoto zaidi yake.

TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari