Like Us On Facebook

ZAIDI YA WATU 40 WAMEFARIKI DUNIA KWENYE AJALI ILYOTOKEA KENYA



Takriban watu 41 wanadaiwa kuuawa baada ya basi moja la abiria lililokuwa likitoka Nairobi kuelekea Homabay Magharibi mwa Kenya kuanguka na kubingirikia mara kadhaa katika eneo la Narok.Polisi wamethibitisha kuwa miongoni mwa waliouawa ni watoto wanne.Mkuu wa polisi wilayani Narok Patterson Maelo amesema kuwa dereva wa basi hilo alishindwa kulithibiti katika eneo la kona na hivyo basi hilo kupoteza mwelekeo na kuanguka.Maafisa wa shirika la msalaba mwekundi ambao tayari wamefika katika eneo la tukio hilo wamesema kuwa watu wengine 33 waliojeruhiwa wamesafirishwa hadi hospitali ya wilaya ya Narok kwa matibabu.Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ni miongoni wa viongozi waliotuma risala zao za rambi rambi kwa jamaa na marafiki wa abiria waliouawa.Katika ripoti iliyochapishwa katika mtandao wake wa twitter, rais Kenyatta ametoa amri kwa idara ya polisi kuchukua hatua dhidi ya wamiliki wa magari ya umma wanaokiuka sheria za barabarani. 
Source:BBC NEWS
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari