Like Us On Facebook

MCHAWI AANGUKA AKIWA KWENYE HARAKATI ZA KUWANGA,ZIMBABWE

Mchawi hivi karibuni kaleta kizaa zaa huko Dzivarasekwa  alipokutwa na 'birthday suit' yake(uchi) 
 Sabina Rokuzhe alikiri kuwa yeye ni mchawi na amedondoka alipokuwa anaruka kwenye ungo akitokea kwenye trip yake ya kuloga huko Masvingo.

Alikutwa kwenye nyumba ya Mbuya Annah Kamupaundi. Akaanza kuwaomba watu waliomzunguka wasimpige ,akasema pia katembelea nyumba kadhaa katika eneo hilo.

Mmoja wao aliyemuona asubuhi mapema ni Mrs Alice Hundi (37) ambae alisema aliamka baada ya kusikia mayowe ya mwanamke kwenye saa nane hivi usiku.

"Nilipomuona yuko uchi,nilimmwagia  chumvi usoni, akaanguka na kuanza kujizungusha zungusha chini. Tuliita polisi na akachukuliwa"

Polisi walitoa uhakika kwamba amechukuliwa na atapewa msaada wa psychiatric.


TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari