Like Us On Facebook

MWANASIASA MMOJA ASHITAKIWA KWA KUMFANANISHA RAIS NA KIAZI

frank 
Mwanasiasa wa Zambia bwana Frank Bwalya ameshtakiwa kwa kosa la kumfananisha rais wa nchi hiyo na kiazi.
Kutokana na mashtaka aliyofunguliwa akikutwa na hatia anaweza kufungwa jela kwa muda wa miaka mitano.
Siku ya Jumatatu akiwa kwenye radio mwanasiasa huyo wa upinzani alimtaja rais wa Zambia kama “chumbu mushololwa” ambapo alikuwa akimfananisha na kiazi.
Mwanasiasa huyo ambaye anatoka National Restoration Party (NRP) ameshafunguliwa mashataka na kesi itaanza kusikilizwa.
Mwaka 2005 kwenye nchi hiyohiyo ya Zambia mwanaume mmoja alifungwa jela miezi 9 kwa kumuabisha kwenye bar rais wa kipindi hicho Levy Mwanawasa.
Mwaka 2002 mhariri wa gazeti moja alikamatwa kwa kumuita Mr Mwanawasa “cabbage” na baadae mashtaka yalifutwa.
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari