Like Us On Facebook

BAADA YA KULEWA POMBE:MREMBO AANZISHA TIMBWILI MANGO GARDEN AKIGOMBEA MPENZI...MATUKIO KATIKA PICHA

Mrembo akizua kasheshe baada ya kutolewa nje ya Ukumbi wa Mango Garden, Mwananyamala, Dar.

AMA kweli pombe siyo chai. Timbwili la aina yake liliibuka ndani ya Ukumbi wa Mango Garden, Mwananyamala jijini Dar hivi karibuni baada ya dada mmoja kuanzisha kasheshe alipomkuta mpenzi wake akiwa amekaa kimahaba na demu mwingine.

Mrembo akiwa mikononi mwa baunsa.
Kisa kizima kilichoshuhudiwa na paparazi wetu kilitokea majira ya saa 8:00 usiku baada ya dada huyo kwenda kujisaidia msalani na aliporudi akamkuta mpenzi wake akiwa ameinamiwa na demu mwingine kimahaba.
...Akitolewa nje ya ukumbi na baunsa.
Dada huyo alipomuona mpenzi wake anamsomesha demu mwingine, hakukubali akamrukia yule demu aliyekuwa akizungumza na mpenzi wake na kuwafanya wote kuanguka chini ndipo timbwili lilipoanza.
 
...Twende nje.
Hata hivyo, timbwili hilo halikudumu kwa muda mrefu kwani walinzi wakiwemo mabaunsa walifanya kazi ya ziada kumtoa dada huyo ukumbini hapo huku akiwa hana viatu.
...Mrembo akitaka kurudi tena.
Hata hivyo, katika kuepusha vurugu zaidi, walinzi wa eneo hilo walimuomba mpenzi wa sistaduu huyo naye atoke nje ili wakamalize ugomvi wao kisha waende wakalale.
...Akizidi kukinukisha.

TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari