Like Us On Facebook

HURUMA:Msanii Geez Mabovu sasa yupo hoi kitandani...!

Geez Mabovu mtoto wa Doll South yuko katika hali mbaya kiafya na amelazwa katika hospitali ya mkoa wa Iringa baada ya kuzidiwa ghafla wakati akisubiri kufanya show mjini humo akiwa na Jan B na Songa. Songa ameandika kwenye ukurasa wake wa facebook kuwaopa taarifa fans wa Mabovu na kuwaomba waendelee kumuombea. “ASANTENI SANA IRINGA,SIKUTEGEMEA MNAPENDA HIP HOP KIASI KILE...MLITISHA SANA. ILA KUNA HABARI MBAYA NDUGU YETU GEEZ MABOVU HALI YAKE SIO NZURI AMELAZWA,NAOMBA TUMUOMBEE ARUDI KATIKA HALI YAKE YA  KAWAIDA. ASANTENI” 
  Geez Mabovu alazwa katika hospitali ya mkoa wa Iringa, tumuombee apone haraka

Songa ameueleza mtandao wa Bongo5 kuwa Mabovu alizidiwa ghafla kabla ya show na akapelekwa hospitali ya mkoa. Mapema jana ,Geez Mabovu aliongea na tovuti ya Times Fm na kueleza kuwa alienda nyumbani kwao Iringa ambapo alikuwa hajaenda kwa muda mrefu na kwamba alienda kusherehekea siku yake ya kuzaliwa (December 25) na familia yake. Rapper huyo aliongeza kuwa ameamua kuacha kutumia pombe kuanzia January Mosi mwakani kutokana na kutaka kufanya mabadiliko zaidi katika maisha yake. Tumuombee Geez Mabovu apate nafuu na apone haraka.
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari