Like Us On Facebook

Zamaradi Mketema azungumzia kilichomfanya aandae filamu ya KIGODORO iliyogharimu milioni 16



Mtangazaji wa kipindi cha Take One cha Clouds TV, Zamaradi Mketema hivi karibuni aliingia msituni kuandaa filamu yake iitwayo ‘Kigodoro’ iliyoshirikisha mastaa wakiwemo Hemedy PHD, Kajala na Muhogo Mchungu.
 
Akiongea na mwandishi wetu, Zamaradi alisema aliamua kuandaa filamu hiyo baada ya kuona kuwa filamu nyingi za Tanzania zina hadithi zile zile hivyo alitaka kuja na kitu tofauti.
 
“Tuna mambo mengi sana ambayo yanaendelea Tanzania ambayo yanaweza kukaa kwenye filamu yakachekesha, yakafurahisha, yakaelimisha. So nikafikiria, nikawaza yale maisha ya uswahilini, watu wanasutana, wanagombana, yale maisha ambayo unakuta chai ipo lakini vitafunio mnajitegemea, nimejaribu kuangaza familia ya aina ile,”alisema Zamaradi.
 
“Nikatoa idea, nikampa mtu aniandikie script, akaandika script vizuri ndo tukaingia mzigoni.”
 
Zamaradi amesema hadi sasa gharama aliyoitumia kutengeneza filamu hiyo ni zaidi ya shilingi milioni 16.
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari