Like Us On Facebook

STEVE RnB WA 'JAMBO JAMBO'AMVISHA PETE MCHUMBA WAKE WA TOKA SECONDARY

Hit maker wa ‘Jambo Jambo’ Steve RnB amefungua ukurasa mwingine wa mapenzi baada ya kumvisha pete ya uchumba mpenzi wake wa siku nyingi ikiwa ni kiashirio cha kuelekea katika ndoa.

Kwa mujibu wa VIBE, Steve ambaye pia ni memba wa bendi ya In Africa amemvisha mpenzi wake huyo anayesemekana kuwa ni wa toka enzi zao za shule.

Kwa picha hii (hapo juu) inaonekana Steve hakutaka kufanya party wala kuifanya kitu kikubwa zaidi ya kuwasilisha ombi lake wakiwa kibarazani na kumwambia kipenzi chake ‘will you marry me’? Hopefully jibu lilikuwa Yes!

Hongera kwa Steve tunawatakia safari njema ya kuelekea kwenye ndoa yeye na mchumba wake.

PICHA: VIBE
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari