Like Us On Facebook

"NIMEPOTEZA MTU MUHIMU SANA MAISHANI".....WEMA SEPETU

MWIGIZAJI wa kike wa filamu mwenye jina kubwa Bongo Wema Sepetu ‘Madam’ hivi karibuni alimpoteza baba yake mzazi aliyefariki katika Hospitali ya TMJ kufuatia msiba huo Wema alifunguka kwa kudai kuwa baba yake kilikuwa ni kiungo muhimu sana katika harakati zake za urembo na sanaa kwa ujumla kwani baba yake alimuunga mkono katika kufanikisha ndoto zake.

Nimepoteza mtu muhimu sana katika maisha yangu baba alikuwa akinisupport katika sanaa kwani hata awali nilipotaka kuingia katika mambo ya ulimbwende baba yangu aliniunga mkono, kulingana na nafasi yake kwa mzazi mwingine isingekuwa rahisi kunikubalia kuingia katika mashindano ya umiss,”anasema Wema.

Wema anasema hadi dakika za mwisho kabla ya baba yake kufariki alikuwa akimwita Miss world, hata alipoingia katika sanaa ya uigizaji wa filamu bado mzazi wake huyo alimuunga mkono jambo ambalo kwake lilikuwa ni faraja na kujivua kuwa na mzazi anayetambua umuhimu wa kipaji cha mwanaye.
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari