Like Us On Facebook

MWENYEKITI CCM ANUSIRIKA KIFO, BAADA YA KUPATA KICHAPO KIKALI TOKA KWA WANAKIJIJI WENYE HASIRA KALI...!! SOMA HAPA KUFAHAMU CHANZO

MWENYEKITIwa Chama Chama Mapinduzi (CCM) Kata ya Kahama Mjini wilayani hapa, Mkoa wa Shinyanga, Febronia Ikombe, amenusurika kifo baada ya kushambuliwa kwa kipigo na jamii ya wafugaji.

 
Mwenyekiti wa Chama Chama Mapinduzi (CCM),Febronia Ikombe.

Mwenyekiti huyo anadaiwa kushambuliwa Jumanne iliyopita saa 5.00 asubuhi katika Kijiji cha Kanegele wilayani Masumbwe mkoa wa Geita baada ya kundi la ng’ombe kuingia kwenye shamba lake la  mpunga na kuharibu mazao.

Akizungumza na waandishi wa habari juzi nyumbani kwake baada ya kutoka hospitali alikokuwa akitibiwa, Ikombe alisema siku ya tukio alipokea taarifa kutoka kwa wakazi wa Kijiji cha Kanegele kwamba kuna ng’ombe wameingia shambani kwake.

Ikombe alisema aliondoka na kwenda shambani akiongozona na watoto wake watatu na dereva wake. Walipofika walikuta ni kweli ng’ombe hao wakiwa shambani. Alisema kutokana na hali hiyo aliwafuata wachungaji wa mifugo hiyo na kuwahoji kwa nini wameingiza mifugo shambani mwake.

Alisema hakupewa jibu, badaka yake mmoja wa wachungaji aliyejulikana kwa jina moja la Mwanasabuni alipiga mayowe hali iliyomshangaza Ikombe.

“Mara niliona kundi la wanakijiji wakija shambani hapo wakiwa na silaha za jadi, fimbo, mapanga na marungu, nilishtuka sana, nikamuuliza Mwanasabuni kwa nini amepiga mayowe, hakunijibu,” alisema.

Alidai wananchi hao baada ya kufika walimshambulia kwa kuwapiga yeye na watoto wake wakitumia fimbo ambapo waliwajeruhi.

“Nimepasuka sehemu ya kushoto karibu na jicho, nilizinduka nikiwa hospitalini ambako nilishonwa nyuzi sita. Mtu aliyenipiga namkumbuka ni mgeni wa mwana kijiji  cha Kanegele. Kwa kweli imenisikitisha sana,” alisema mwenyekiti huyo.


TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII
KAMA UMEGUSWA NA HABARI ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
 

KILELE CHA HABARI Copyright © 2014 -- Template created by Mbatta -- Powered by Kilelechahabari